Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 2 2022-04-05

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KUNTI Y. MAJALA K.n.y. MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Ivuna hadi Chole ili kurahisisha mawasiliano kati ya Wilaya ya Momba na Songwe?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stella Simon Fiyao, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Ivuna hadi Chole yenye urefu wa kilomita 18.5 ni barabara muhimu iliyopo Wilaya ya Momba ambayo inaungainisha barabara ya Muheza hadi Isanzu yenye urefu wa kilomita 12 katika Wilaya ya Songwe. Ili kuunganisha Wilaya hizi mbili jumla ya kilometa 30.50 zinatakiwa kufanyiwa matengenezo.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/ 2023, Serikali itatenga jumla ya Shilingi Milioni 200 kwa ajili ya ujenzi wa daraja lenye urefu wa mita 200 katika barabara ya Ivuna – Chole Wilaya ya Momba na kwa upande wa Wilaya ya Songwe Shilingi Milioni 100 kwa ajili ya kufanya matengenezo yenye urefu wa kilomita 3 katika barabara hiyo.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya barabara katika barabara hii yenye urefu wa kilometa 30.5 kulingana na upatikanaji wa fedha.