Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Ifakara watapewa fedha za ujenzi wa Soko la Halmashauri ya Mji wa Ifakara ambao umesuasua kwa muda sasa?

Supplementary Question 1

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na kwa kuzingatia maelekezo yako ya maswali ya nyongeza yawe mafupi, nakushukuru sana swali langu kuwa la kwanza katika Bunge lako hili la kwanza ikiwa Simba imeshafanya yake. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, wakati Simba ikifanya yao tayari Yanga Sport Club ikiwa inaongoza ligi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Sasa naomba kuuliza maswali yangu mafupi madogo mawili ya nyongeza.

Kwanza, kwa kuzingatia majibu ya Mheshimiwa Waziri ni kwamba tumekosa fedha kutokana na ripoti ya wataalam wetu au andiko la wataalam wetu kutokukidhi vigezo. Je, Mheshimiwa Waziri anatuhakikishia kwamba ataweza kutupatia wataalam ili tuandike upya andiko hili?

Swali la pili, wananchi wa Mji wa Ifakara wanateseka sana kutokana na soko hasa msimu huu wa mvua. Je, Mheshimiwa Waziri mwenyewe wa TAMISEMI atakuwa tayari katika Bunge hili kutafuta hata siku moja kutembelea soko hili na kuzungumza na wananchi wa Mji wa Ifakara?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Abubakari Damian Asenga, Mbunge wa Jimbo la Kilombero kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza aliuliza kwamba kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI tunaweza kuwapatia wataalam. Tuko tayari kuwapatia wataalam ambao watashirikiana na Halmashauri ya Mji wa Ifakara kuhakikisha wanakamilisha andiko lao, kwa hiyo hilo tuko tayari.

Mheshimiwa Spika, swali la pili kuhusu kwenda Ifakara. Mheshimiwa Mbunge mimi niko tayari hususani wakati wa weekend tunaweza tukaongozana kwenda kushuhudia hiyo kero ya wananchi katika eneo lako. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Ifakara watapewa fedha za ujenzi wa Soko la Halmashauri ya Mji wa Ifakara ambao umesuasua kwa muda sasa?

Supplementary Question 2

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuwa hali ilivyo Kilombero inafanana kabisa na ilivyo katika Jimbo la Sumve katika eneo la Bungulwa ambapo Halmashauri tumeshaleta andiko la kujenga soko la kisasa katika mnada wa Bungulwa.

Je, Serikali haioni sasa kuna umuhimu wa kuleta pesa ili mradi huu muhimu kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba ufanyike?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kasalali, Mbunge wa Sumve, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, anasema Halmashauri yake imeshaleta andiko katika ofisi ya Rais, TAMISEMI, kwa sasa anachohitaji tu ni kwamba fedha sasa itolewe kwa ajili ya soko hilo. Mimi tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaenda kupitia hilo andiko na kuangalia namna bora ambayo tunaweza tukatafuta fedha kuhakikisha kwamba tunaleta katika Halmashauri yake.

Mheshimiwa Spika, hiyo ndiyo commitment ya Serikali, ahsante.(Makofi)