Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 1 2022-04-05

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: -

Je, ni lini wananchi wa Ifakara watapewa fedha za ujenzi wa Soko la Halmashauri ya Mji wa Ifakara ambao umesuasua kwa muda sasa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abubakari Damian Asenga, Mbunge wa Jimbo la Kilombero kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa Halmashauri ya Mji wa Ifakara kuwa na Soko la Kisasa ili kuboresha mazingira ya wafanyabishara wa Mji wa Ifakara na kuongeza mapato ya Halmashauri hiyo.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2018/2019 Halmashauri ya Mji wa Ifakara iliandaa na kuwasilisha Serikali Kuu andiko la mradi wa kimkakati wa ujenzi wa soko hilo kwa gharama ya shilingi bilioni 14.3 ambalo halikukidhi vigezo. Hivyo, Halmashauri ya Mji wa Ifakara inahimizwa kuweka kipaumbele na kutenga fedha kwenye bajeti yao ili kukamilisha andiko la mradi huo ambalo litawezesha kutafauta fedha za kutekeleza mradi huo.