Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nancy Hassan Nyalusi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI K.n.y. MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, lini skimu za umwagiliaji Ukanda wa joto Ihowanza, Malangali, Idunda, Mbalamaziwa, Itandulu, Nyololo na Maduma zitajengwa?

Supplementary Question 1

MHE. NANCY H. NYALUSI: Mheshimiwa Spika, skimu ya umwagiliaji ya Mgololo ambayo ina hekta 700 ilijengwa na Serikali kwa shilingi bilioni 1.9 ambayo ilikamilika mwaka 2012, mwaka 2013 ikaanza kutumika na mwaka 2013 hiyo hiyo mifereji ikaanza kuvujisha maji kwa sababu ilikuwa ni mibovu.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kumaliza kujenga mifereji hiyo ili kuokoa pesa yake iliyotolewa, lakini pia kwa sababu mradi huo haujakamilika na haujawanufaisha wananchi? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Nancy Nyalusi, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Skimu hii ya Mgololo ni muhimu kwa sababu inahusisha Kata mbili za Makungu na Kiyowela na humo ndani kuna vijiji zaidi ya tisa ambavyo vinanufaika na mradi huu. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika bajeti yetu inayokuja tutauingiza mradi huu kwa ajili ya utekelezaji ili kuweza kurekebisha mapungufu yote na uweze kuwanufaisha wananchi, hasa wa Vijiji vya Lugolofu, Kitasengwa, Lugema, Mabaoni, Makungu na Lole.

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI K.n.y. MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, lini skimu za umwagiliaji Ukanda wa joto Ihowanza, Malangali, Idunda, Mbalamaziwa, Itandulu, Nyololo na Maduma zitajengwa?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi; je, Serikali itajenga lini skimu ya umwagiliaji katika Bonde la Eyasi ili kuboresha kilimo cha umwagiliaji unaoendelea kwenye bonde hilo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Daniel Awack Tlemai kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika bajeti yetu ya mwaka huu wa fedha Skimu za Eyasi zimebainishwa kuwa ni sehemu ya utekelezaji katika bajeti hii na katika utekelezaji wa mradi huo hivi sasa tupo katika hatua ya manunuzi ya kumpata mkandarasi ili utekelezaji uanze mara moja.

Name

Twaha Ally Mpembenwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI K.n.y. MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, lini skimu za umwagiliaji Ukanda wa joto Ihowanza, Malangali, Idunda, Mbalamaziwa, Itandulu, Nyololo na Maduma zitajengwa?

Supplementary Question 3

MHE. TWAHA A. MPEMBENWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ni nini mkakati wa Serikali wa kuwasaidia wananchi na wawekezaji katika Kata ya Mtunda kwenye Jimbo la Kibiti katika miundombinu ya umwagiliaji ukizingatia kwamba kuna uwekezaji mkubwa sana wa kilimo cha mpunga umefanyika pale na unaendelea wa ekari zisizopungua 20,000?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Twaha Mpembenwe, Mbunge wa Kibiti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo tumekuwa tukisema hapa tunatambua kwamba Bonde la Rufiji ni kati ya mabonde muhimu katika kilimo cha umwagiliaji hapa nchini Tanzania na ndiyo maana katika mkakati wetu wa mwaka huu katika bajeti yetu, tumeamua kuyapitia mabonde yote 22 likiwemo Bonde la Rufiji kwa lengo la kuhakikisha kwamba tunafanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili baadaye tuje tutekeleze miradi mikubwa ya umwagiliaji ambayo pia itawagusa wananchi wa Mheshimiwa Mbunge.

Name

Kenneth Ernest Nollo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI K.n.y. MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, lini skimu za umwagiliaji Ukanda wa joto Ihowanza, Malangali, Idunda, Mbalamaziwa, Itandulu, Nyololo na Maduma zitajengwa?

Supplementary Question 4

MHE. KENNETH E. NOLLO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa na mimi nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Skimu ya Kongogo ni moja ya skimu ambazo ziliwekwa kwenye bajeti ya 2022/2023; je, Serikali imefikia wapi katika kuanza utekelezaji wa ujenzi wa skimu hiyo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kenneth Nollo, Mbunge wa Bahi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Skimu ya Kongogo ipo katika bajeti ya mwaka huu na hatua ambayo tumeifikia, mkandarasi ameshapatikana na muda wowote kuanzia hivi sasa atakwenda kuanza utekelezaji wa ujenzi wa skimu hiyo.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI K.n.y. MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, lini skimu za umwagiliaji Ukanda wa joto Ihowanza, Malangali, Idunda, Mbalamaziwa, Itandulu, Nyololo na Maduma zitajengwa?

Supplementary Question 5

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, Skimu ya Arusha Chini iliyopo Halmashauri ya Mji wa Nanyamba ni miongoni mwa skimu ambazo zitafanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu kwa mwaka huu wa fedha; je, ni lini kazi hiyo itaanza?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Nanyamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli skimu hii ilibainishwa na kuwekwa katika mpango wetu wa utekelezaji katika mwaka huu wa fedha. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba hivi sasa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imeendelea kufanya kazi ya kukamilisha taratibu zote kwa ajili ya manunuzi na hatua nyinginezo ili kazi hizi zianze kwa uharaka.

Mheshimiwa Spika, kufikia Disemba mwaka huu tutakuwa tumefika hatua kubwa sana katika miradi yote, na hivyo nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba katika kipindi hiki cha muda mfupi, eneo lake hilo pia litajumuishwa na tutaanza kazi hiyo ya usanifu na upembuzi.

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI K.n.y. MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, lini skimu za umwagiliaji Ukanda wa joto Ihowanza, Malangali, Idunda, Mbalamaziwa, Itandulu, Nyololo na Maduma zitajengwa?

Supplementary Question 6

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwenye Mradi wa Songwe River Basin kuna package inayounganisha eneo la umwagiliaji la hekta zaidi ya 3,500 pale Kyela.

Je, Serikali imefikia wapi kuungana na Malawi kuanza kutekeleza mradi huu?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Mlaghila Jumbe, Mbunge wa Kyela, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema muuliza swali, Mheshimiwa Mbunge, amelitaja Bonde la Mto Songwe ambalo ni sehemu ya utekelezaji wa mradi huu. Kazi ambayo Wizara inafanya hivi sasa ni kuhakikisha tunaendelea na kazi ya upembuzi yakinifu wa haya mambonde yote, lengo letu kubwa ni kuwa na miradi mikubwa ambayo itahusisha miradi ambayo pia Mheshimiwa Mbunge ameitaja.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo mwaka huu wa fedha tayari tumeshawapa kazi washauri elekezi kwa ajili ya kuanza kazi hii na tunategemea kwamba mabonde yote yale 22 kuanzia Bonde la Ziwa Victoria, Malagarasi, Manonga, Wembele, Bonde la Ruvuma, Bonde la Rufiji, Bonde la Mto Songwe, Ifakara Idete, Kilombero, Mkomazi, haya yote yapo katika mpango na yatakwenda kukata kiu ya wakulima wa Tanzania. (Makofi)

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI K.n.y. MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, lini skimu za umwagiliaji Ukanda wa joto Ihowanza, Malangali, Idunda, Mbalamaziwa, Itandulu, Nyololo na Maduma zitajengwa?

Supplementary Question 7

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, nafurahi sana.

Je, Mheshimiwa Waziri anaweza akaniambia ni lini ukarabati wa skimu zilizo kwenye Kata ya Kahe Magharibi na mifereji iliyo kwenye Kata za Marangu Mashariki, Kirua Vunjo na Kilema utafanyika?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Charles Stephen Kimei, Mbunge wa Vunjo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tuna orodha ya miradi mingi sana ambayo mwaka huu wa fedha tunaifanyia kazi. Hivyo, nitaomba mimi na Mheshimiwa Mbunge tukae tuangalie maeneo ambayo tutayafanyia utekelezaji mwaka huu katika Mkoa wa Kilimanjaro ni yapi, na ya mwaka unaokuja ni yapi, ili kama hayapo katika mwaka huu wa fedha basi tuyaingize kwa ajili ya mwaka ujao wa fedha. Lakini lengo letu ni kuhakikisha mifereji yote hii inafanyiwa kazi na wakulima wa kutoka Jimboni kwa Mheshimiwa Kimei wanapata fursa ya kilimo cha umwagiliaji.

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI K.n.y. MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, lini skimu za umwagiliaji Ukanda wa joto Ihowanza, Malangali, Idunda, Mbalamaziwa, Itandulu, Nyololo na Maduma zitajengwa?

Supplementary Question 8

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Spika, Skimu ya Umwagiliaji ya Kidoka ni kati ya skimu zilizopo kwenye Mkoa wa Dodoma, lakini skimu ile miundombinu yake imekuwa chakavu na wakulima wetu wamekuwa wakijiendesha kwa hasara sana kutokana na gharama kubwa za umeme wanazozitumia ku-pump maji.

Je, ni lini sasa Serikali mtakwenda kuweka miundombinu rafiki ya skimu ile ili wananchi wetu waweze kujiendesha vizuri kwa faida? Ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kunti Yusuph Majala, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dodoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja kati ya kazi kubwa ambazo tuliwapa watu wa tume ni kuhakikisha wana-take stock ya miradi yote ambayo imekwama na yenye changamoto, na tumekamilisha zoezi hilo. Hivi sasa ni kuanza kupitia na kuona namna gani tunaweza tukaboresha skimu hizo.

Mheshimiwa Spika, nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba nitatoa maelekezo kwa watu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kuhakikisha Jumatatu wawepo katika eneo la Kidoka kuangalia changamoto ni ipi na tuone namna ya kuweza kurekebisha skimu hiyo.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI K.n.y. MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, lini skimu za umwagiliaji Ukanda wa joto Ihowanza, Malangali, Idunda, Mbalamaziwa, Itandulu, Nyololo na Maduma zitajengwa?

Supplementary Question 9

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Kalenga lina skimu 19 na nyingi ni chakavu; je, ni lini sasa Serikali itatenga bajeti kwa ajili ya ukarabati huo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jackson Gedion Kiswaga, Mbunge wa Kalenga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema wakati najibu swali la Mheshimiwa Kunti, tunayo stock ya miradi yote ambayo ina changamoto na nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaingiza miradi yake pia katika mpango wetu na tutaipitia kuona inahitaji marekebisho gani.

Mheshimiwa Spika, lakini lengo letu kubwa hasa; sisi tulifanya kazi ya kupitia miradi yote, tunataka tufanye kilimo cha umwagiliaji kwa hiyo hatutaliacha eneo lolote, tutayafikia maeneo yote. Lengo letu ni kwenda katika kilimo cha umwagiliaji. Kwa hiyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge.

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. NANCY H. NYALUSI K.n.y. MHE. DAVID M. KIHENZILE aliuliza: - Je, lini skimu za umwagiliaji Ukanda wa joto Ihowanza, Malangali, Idunda, Mbalamaziwa, Itandulu, Nyololo na Maduma zitajengwa?

Supplementary Question 10

MHE. FRANCIS L. MTEGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Wakulima wa skimu za umwagiliaji Matebete, Chosi, Herman, Isenyela wanapata shida sana wakati wa uhaba wa mvua kwa kupeana zamu usiku, na wengi wao wanazunguka na mapanga usiku kucha.

Je, Serikali itawaboreshea skimu hizi lini ili kuondoa adha hii na waweze kulima kwa tija?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika eneo la Mbarali tuna miradi ya umwagiliaji ambayo tumeitengea fedha ya kiasi cha shilingi bilioni 61 ambayo inahusisha Herman Chosi, Bonokuva Gigolo na kwenda katika Matebete, tunakwenda Ifenyela na Uturo. Haya yote niliyoyataja wakandarasi wameshapatikana na muda wowote kazi ya utekelezaji wa miradi hii unaanza.