Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY: aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme katika maeneo ya Tarafa za Jimbo la Mbulu za Manetadu, Tumatu Arri, Masieda na Yayeda chini?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa muda wa kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa umeme umefika Dongobesh miaka 11 iliyopita na haujawahi kwenda kijiji hata kimoja na pia miaka ya tisini umefika Haydom. Je, Serikali iko tayari sasa kusogeza umeme huo kutoka Kata hizo ambazo nimezisema kuelekea kwenye Kata ambazo amezitaja? (Makofi)
Swali la pili, kwa kuwa tuna miradi ambayo ni ya maji, na inahitaji umeme na kwenye REA phase two, hatujawahi kupata mradi huo: Je, Serikali iko tayari kukubali sasa kuanza na Vijiji hivi vya Kata ya Hayderer, Getanyamba, Dinamu, Maretadu, Masieda, Laba na Dinamu?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa, Serikali iko tayari kusogeza umeme kwenye Vijiji alivyotaja Mheshimiwa Mbunge. Nikiri kwanza Vijiji ambavyo amevitaja kwa lugha yangu, naweza nisivitamke kwa usahihi, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hata Vijiji mbavyo amevitaja ambavyo havikuwa kwenye REA Awamu ya Pili, tunaviingiza kwenye REA Awamu ya Tatu.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, pamoja na REA, Awamu ya Pili inayokamilika na REA, Awamu ya Tatu inayoanza, tutampelekea pia mradi mwingine wa kusambaza ma-transformer ili kuhakikisha Vijiji ambavyo viko karibu na Vijiji vilivyopewa umeme na vyenyewe vitapata umeme. Lengo ni kuvipatia Vijiji vyako vyote umeme kwenye REA, Awamu ya Tatu.