Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 22 Energy and Minerals Wizara ya Madini 192 2016-05-18

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY: aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme katika maeneo ya Tarafa za Jimbo la Mbulu za Manetadu, Tumatu Arri, Masieda na Yayeda chini?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inagharamia utekelezaji wa mradi kabambe wa kusambaza umeme vijijini (REA), kupitia mpango huu wa REA Vijijini (REF). Mradi huu unatekelezwa katika mikoa yote ya Tanzania Bara ikiwemo Mkoa wa Manyara. Mkandarasi, CC International Nigeria Limited, hivi sasa anaendelea na utekelezaji wa mradi huo katika Wilaya za Mkoa wa Manyara ikiwemo Wilaya ya Mbulu Vijijini. Utekelezaji wa mradi huu umefikia asilimia 84, ambapo tayari transformer zimeshafungwa na pia wateja 354 wameunganishiwa umeme katika Mkoa mzima wa Manyara.
Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huu unategemea pia kukamilika mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu 2016. Lengo kubwa la mradi huu ni kupeleka huduma za umeme kwa wananchi na hivyo kurahisisha shughuli za kiuchumi pamoja na kijamii. Tarafa za Manetatu, Masieda, Tumatiadi na Yaeda Chini zimejumuishwa katika Mpango wa Usambazaji wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu, utakaoanza mara baada ya bajeti ya mwaka huu 2016/2017.