Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kutoka Singida hadi Sepuka kuelekea Kizaga itajengwa kwa kiwango cha lami katika Wilaya ya Ikungi?

Supplementary Question 1

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri swali nyongeza kwamba kwa kuwa barabara hii ilitajwa kwenye Ilani ya Uchaguzi wa mwaka 2015/2020 haikutekelezwa; ikatajwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya 2020/2025 na mpaka sasa hivi tunavyozungumza bado hakuna mchakato wowote wa barabara hii.

Nini kauli ya Serikali kwa wananchi wa Jimbo la Singida Magharibi na wananchi wa Mkoa wa Singida na Iramba kwa ujumla juu ya barabara hii? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Elibariki Immanuel Kingu, Mbunge wa Singida Magharibi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kauli ya Serikali na kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi na kama alivyosema imetamkwa kwenye Ilani, Serikali inasema inategemea kutangaza zabuni kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami mwishoni mwa mwezi huu wa kumi na mbili kwa ajili ya kuanza kuijenga yote kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kutoka Singida hadi Sepuka kuelekea Kizaga itajengwa kwa kiwango cha lami katika Wilaya ya Ikungi?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Makambako - Songea tunajua kipande cha Songea mpaka mpaka na Njombe tayari kimeishapata mpango wake. Lakini kutoka mpakani mwa Songea na Njombe mpaka Makambako Serikali ina mkakati gani kuhusiana na kipande hiki cha barabara?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutafuta fedha kufanya matengenezo makubwa kwa barabara yote ya Makambako - Njombe hadi Songea. Kwa sasa kama alivyosema mpakani mwa Njombe na Ruvuma tayari tumeishapata fedha na Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kufanya matengenezo makubwa kwa kipande ambacho kimeharibika sana kati ya Makambako - Njombe hadi mpakani mwa Mkoa wa Ruvuma, ahsante. (Makofi)

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kutoka Singida hadi Sepuka kuelekea Kizaga itajengwa kwa kiwango cha lami katika Wilaya ya Ikungi?

Supplementary Question 3

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi.

Je, Serikali ina mpango gani wa barabara ya kuunganisha Mkoa wa Singida na Mkoa wa Simiyu kupitia Daraja la Sibiti?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Singida na Mkoa wa Simiyu kupitia Daraja la Sibiti hivi ninavyoongea barabara zote tatu ziko kwenye kukamilisha usanifu wa kina kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami kuanzia Ulemo kwenda Sibiti, lakini pia kuanzia Iguguno kwenda Sibiti wakandarasi wako tayari wanafanya usanifu kwa ajili ya maandalizi ya kujenga kwa kiwango cha lami kuunganisha hiyo mikoa miwili, ahsante.

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kutoka Singida hadi Sepuka kuelekea Kizaga itajengwa kwa kiwango cha lami katika Wilaya ya Ikungi?

Supplementary Question 4

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Je ni lini barabara ya Karatu - Njia Panda kwenda Mang’ola - Matala hadi Lalago ambayo pia ipo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya 2020 itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyotaja kutoka Karatu - Mang’ola hadi Sibiti ni barabara kuu. Hata hivyo tumeisha kamilisha usanifu na Serikali inaendelea kutafuta fedha kuijenga hiyo barabara ambayo inapita sehemu muhimu sana ya uchumi na hasa kilimo cha vitunguu, ahsante.

Name

Shabani Hamisi Taletale

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kutoka Singida hadi Sepuka kuelekea Kizaga itajengwa kwa kiwango cha lami katika Wilaya ya Ikungi?

Supplementary Question 5

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kuiuliza Serikali; je, ni lini barabara yetu ya Bigwa - Kisaki ya kilometa 78 itaanza matengenezo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Taletale, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara hii ilitangazwa, lakini kilometa zilikuwa chache na sasa barabara hii tunategemea kuitangaza muda wowote kuijenga kwa kiwango cha lami na tuko kwenye hatua za mwisho za manunuzi na barabara hii nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge itatangazwa mwaka huu wa fedha na itaanza kujengwa hizo kilometa 78, ahsante.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kutoka Singida hadi Sepuka kuelekea Kizaga itajengwa kwa kiwango cha lami katika Wilaya ya Ikungi?

Supplementary Question 6

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona; barabara ya kutoka Kibena kwenda Madeke barabara hii ipo kwenye Ilani na Mheshimiwa Rais, juzi alisema barabara hii itajengwa kwa lami na Mbunge wa Lupembe amekuwa akizungumza mara kwa mara. Nini kauli ya Serikali juu ya barabara ya Kibena - Madeke? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Sanga, Mbunge wa Makambako, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kuna maelekezo ambayo tumeyapata kwamba barabara hii ya Kibena junction - Madeke hadi Mlimba, Ifakara ijengwe kwa kiwango cha lami. Upande wa Morogoro ambako inakwenda tayari tumeshatangaza zabuni na upande wa Kibena kwenda Madeke ipo kwenye usanifu chini ya African Development Bank, lakini pia tunategemea tuanze kuijenga kwa kilometa chache kuanzia mwaka huu wa fedha, ahsante. (Makofi)