Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 10 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 146 2022-11-11

Name

Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. ELIBARIKI I. KINGU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kutoka Singida hadi Sepuka kuelekea Kizaga itajengwa kwa kiwango cha lami katika Wilaya ya Ikungi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Elibariki Immanuel Kingu, Mbunge wa Singida Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha usanifu wa kina na maandalizi ya nyaraka za zabuni kwa barabara ya Sabasaba – Sepuka – Ndago hadi Kizaga yenye urefu wa kilometa 77.6 na inategemea kutangaza zabuni kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami mwishoni mwa mwezi Novemba, 2022. Ahsante.