Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kusambaza vipimo vya maabara hasa vya malaria katika zahanati za Mtwara Vijijini?

Supplementary Question 1

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, bado kuna changamoto kubwa ya ukosefu wa wataalam wa kusoma vipimo hivi; je, Serikali ina mpango gani wa kutuletea wataalam hao?

Swali langu la pili; je, Serikali haioni umuhimu wa kutusambazia vipimo vikubwa kwenye zahanati zetu pamoja na hospitali yetu ya Wilaya Nanguruwe ili tuweze kupima na magonjwa mengine? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Shamsia Azizi Mtamba, Mbunge wa Jimbo la Mtwara Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, jambo la kwanza nimuondoe hofu, kadri Serikali itakavyoendelea kuajiri na kuongeza wataalam katika kada ya afya maana yake na mgawanyo huo utafika mpaka katika Jimbo lake la Mtwara Vijijini na maeneo mengine ya Taifa. Kwa hiyo, lipo katika mpango wa Serikali na tunaendelea kuajiri kila mwaka.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, umuhimu wa kuongeza vipimo vikubwa hilo lipo na ndiy kazi kubwa anayofanya Rais wa sasa Mama yetu Samia Suluhu Hassan. Sasa hivi Ofisi ya Rais – TAMISEMI tukishirikiana na Wizara ya Afya, tunatarajia kupokea shilingi bilioni 169.7 kutoka Benki ya Dunia kwa ajili ya ununuzi wa vifaa, vifaa tib ana vitendanishi kwa ajili ya maabara. Kwa hiyo tutaendeela kuvileta kwa kadri ambavyo vinapatikana. Ahsante sana.