Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 10 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 143 2022-11-11

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kusambaza vipimo vya maabara hasa vya malaria katika zahanati za Mtwara Vijijini?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shamsia Azizi Mtamba, Mbunge wa Jimbo la Mtwara Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Septemba, 2022, kipimo cha Malaria (mRDT), kuna vitepe vya kutosheleza matumizi ya miezi mitano na kabla ya kufika tarehe 30 Desemba, 2022 Bohari Kuu ya Dawa inategemea kupokea shehena nyingine ya vitendanishi hivyo vya malaria. Aidha, hali ya upatikanaji wa vitendanishi vya vipimo vya malaria katika Kanda ya Mtwara kufikia Oktoba, 2022 ni vitepe 631,825 ukilinganisha na matumizi ya vitepe hivyo ambavyo ni 84,150 kwa mwezi katika Kanda ya Mtwara, hivyo kuna shehena ya kutosheleza miezi saba ijayo.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais, TAMISEMI inaendelea kuwakumbusha watumishi wanaohusika kuandaa taarifa na kuomba vitendanishi kwa ajili ya vipimo hivyo, kufanya maoteo kwa usahihi na kuomba kwa wakati maana vitendanishi hivyo vipo vya kutosha MSD Makao Makuu na kwenye Kanda husika.