Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawatafutia wakulima wa Kishapu Masoko ya Mazao ya Mtama na Uwele?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; changamoto bado ni kubwa sana hususani soko la ndani kwa wakulima wa zao la mtama na uwele. Je, Serikali ina utaratibu gani wa kuhakikisha kwamba yenyewe inashughulika kununua mazao haya kupitia NFRA ili mradi kupunguza tatizo la changamoto ya soko la ndani?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kuna tatizo kubwa la ndege aina ya kwelea kwelea ambao wamekuwa wakishambulia sana mazao haya ya mtama pamoja na uwele na Serikali yetu ina tatizo la kutokuwa na ndege ambayo ni maalum kwa ajili ya kushughulikia ndege hawa waharibifu wa mazao haya. Je, Serikali haioni haja ya kuhakikisha kwamba inanunua ndege yake ili mradi iweze kushughulika kwa karibu na ndege hawa waharibifu ambao wanashambulia mazao haya?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Nyangindu Boniphace Butondo, Mbunge wa Kishapu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, la kwanza, namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa namna ambavyo amekuwa akiwapambania na kuwasemea wakulima wa mtama pamoja na uwele kutoka Mkoa wa Shinyanga.

Mheshimiwa Spika, kuhusu uhakika wa soko la ndani, maelekezo tayari NFRA wanayo ya kununua mazao hayo ikiwemo mtama pamoja na uwele. Kwa hiyo nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba NFRA anaendelea na zoezi la kununua mtama hivyo wakulima wa Shinyanga ni sehemu ya wanufaika wa soko hili la ndani kupitia NFRA.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, kuhusiana na ndege. Katika bajeti yetu ya mwaka huu tumetenga Shilingi bilioni tatu ya kununua ndege mpya kwa ajili ya kunyunyizia wadudu kwenye sehemu ya kukuza kilimo anga. Ninavyozungumza hivi sasa tuko katika due diligence, tunazo kampuni tatu, mbili kutoka Marekani na moja kutoka Afrika ya Kusini ambako baadaye sasa tutafanya maamuzi ni wapi tununue ndege hiyo.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo, tunayo ndege yetu pia ya survey ambayo iko Nairobi Kenya, imekamilishwa matengenezo yake na yenyewe pia itakuja kuungana kuimarisha kilimo anga ili kuondokana na changamoto hii ya wadudu waharibifu.