Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 6 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 84 2022-11-07

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawatafutia wakulima wa Kishapu Masoko ya Mazao ya Mtama na Uwele?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Boniphace Nyangindu Butondo, Mbunge wa Kishapu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na ongezeko la mahitaji ya zao la mtama na uwele kwa ajili ya matumizi ya viwanda vya ndani ya nje ya nchi. Kutokana na ongezeko la mahitaji hayo, Serikali inatekeleza mikakati mbalimbali kuhakikisha wakulima wa mazao hayo wanapata masoko ya uhakika.

Mheshimiwa Spika, mikakati hiyo ni pamoja na kuzalisha mbegu bora zinazokidhi mahitaji ya soko, kuwaunganisha wakulima na wanunuzi wa ndani kama TBL ambao wameanza kununua mazao hayo katika Mikoa ya Dodoma na Manyara na kufungua Vituo vya Mauzo katika Mji wa Juba, Sudan Kusini na Lubumbashi Nchini Congo.