Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kuzuia nyavu haramu?

Supplementary Question 1

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, naomba niwe na maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza: Kwa kuwa nyavu nyingi zinaagizwa kutoka nje ya nchi na kuingizwa ndani ya nchi, lakini mwisho wa siku, mvuvi ndio amekuwa mhanga mkubwa wa hizi nyavu: Je, Serikali imewahi kuwawajibisha watendaji wengine kama ilivyowataja kwenye swali la msingi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili: Serikali ina mkakati gani wa kuwawezesha wavuvi kupata vifaa vya kisasa ili waondokane na zana za uvuvi zilizopitwa na wakati?

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Eng. Stella Simon Fiyao, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali kuhusu je, wapo ambao wamewahi kuwajibishwa kutokana na kwamba nyavu hizi huwa zinaagizwa kutoka nje au zinazalishwa na watu, wapo? Zipo kesi kadhaa ambazo zimewahusisha waagizaji na zilizowahusisha watengenezaji na kesi hizi zote tulipokwenda Mahakamani Serikali ilifaulu kwa kushinda kesi zile. Zipo kesi nyingine ambazo hata sasa bado zinaendelea. Wako watendaji ambao walichukuliwa hatua mbalimbali na wengine kesi zao bado ziko Mahakamani.

Mheshimiwa Spika, swali la pili alitaka kujua juu ya uwezeshaji wa makundi ya wavuvi kwa kupata vifaa vya kisasa. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama yetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan na Serikali yetu ya Awamu ya Sita. Tunayo program kubwa ambayo inaendelea hivi sasa ya kuhakikisha kwamba tunakwenda kukopesha boti za kisasa takribani 150 hadi 160 kwa wavuvi wote nchini, wale watakaokidhi vigezo. Boti hizi zitakuwa na vifaa kama vile fish finder kwa maana ya kile kifaa cha kujua Samaki walipo, vilevile eneo la kuhifadhia samaki takribani tani moja hadi tani moja na nusu, GPS na zitakuwa zimeunganishwa katika Satelite ili mvuvi kabla hajatoka kwenda katika uvuvi awe tayari na picha ya kujua mahali walipo samaki. Ahsante.