Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zahor Mohamed Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwera

Primary Question

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI aliuliza: - Je, vikao vinavyopokea na kujadili changamoto za Muungano bado vipo na lini vilikaa mara ya mwisho?

Supplementary Question 1

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI: Mheshimiwa Spika, naomba nikushukuru kwa kunipa nafasi hii. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, ambayo yamesema kikao chamwisho kilifanyika Agosti, 2021 na katika kikao hicho changamoto 11 kati ya 18 zilipatiwa ufumbuzi.

(a) Je, Serikali inaweza kulitaarifu Bunge sasa mambo hayo ni yapi?

(b) Ni lini Serikali italeta Muswada ili mambo yaya sasa yatambulike kisheria kwamba yapo nje ya changamoto zetu na kila mtu afanye ya kwake?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zahor Mohammed Haji, Mbunge wa Jimbo la Mwera, kama iifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika changamoto 25, jumla ya changamoto 28 zimeshapatiwa ufumbuzi, miongoni mwa hizo kama ambavyo umenishauri nitampelekea kwa maandishi ili aweze kuziona. Zipo changamoto kwa mfano kulikuwa kuna hoja ya uvuvi katika Bahari Kuu hii ilishapatiwa ufumbuzi, kulikuwa kuna hoja ya mgawanyo wa mapato ilishapatiwa ufumbuzi. Kulikuwa kuna hoja ya mapato yanayotokana na uhamiaji, hii ilishapatiwa ufumbuzi kwa upande wa Zanzibar, kulikuwa kuna hoja ya ucheleweshaji wa miradi ya maendeleo, kusainiwa kwa mikataba ya miradi ya maendeleo Zanzibar hili limeshapatiwa ufumbuzi.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano kusainiwa kwa mkataba ujenzi wa Hospitali ya Mbiguni Zanzibar, ukarabati wa Hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar, ujenzi wa barabar ya kutokea Chake, Machomanne, Meli Tano kuelekea kwa Binti Abeid kueleka Wete, yote haya na mengine yalishapatiwa ufumbuzi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mengine kama ulivyoshauri nitampelekea kwa maandishi.

Mheshimiwa Spika, suala lingine ni kuwa jambo hili la Muungano ni jambo ambalo hati zake zimesainiwa zipo na zina nguvu kisheria. Kwa hiyo, nimuambie tu Mheshimiwa Mbunge, kwa sababu ni jambo ambalo linahitaji ridhaa ya pande zote mbili, wacha tukakae tutakapoona kuna haja ya kuleta kama Muswada basi tutalileta hapa. Nashukuru. (Makofi)