Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 6 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 71 2022-11-07

Name

Zahor Mohamed Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwera

Primary Question

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI aliuliza: -

Je, vikao vinavyopokea na kujadili changamoto za Muungano bado vipo na lini vilikaa mara ya mwisho?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Zahor Mohammed Haji Mbunge wa Mwera kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, napenda kulitaarifu Bunge lako Tukufu kuwa kuwa vikao vya kupokea na kujadili changamoto za Muungano bado vipo na vitaendelea kuwepo kutokana na umuhimu wake kwa mustakabali wa Muungano wetu.

Mheshimiwa Spika, napenda pia kulitaarifu Bunge kuwa, kwa mwaka 2021/2022 vikao hivyo vilifanyika kwa mujibu wa mwongozo huo ambapo kikao cha Kamati ya pamoja ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SJMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) ya kushughulikia Masuala ya Muungano kilifanyika Tarehe 24 Agosti, 2021. Mheshimiwa Spika, ninakushukuru.