Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. JEREMIAH M. AMSABI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kusaidia Hospitali ya Wilaya ya Serengeti na Nyerere DHH kwa kuzijengea uwezo wa kutoa huduma bora?

Supplementary Question 1

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana na naishukuru Serikali kwa majibu mazuri. Pamoja na hayo niombe kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; katika bilioni 2.36 ambazo zilipelekwa Hospitali ya Wilaya, zilichukuliwa milioni 400 ambazo zilikuwa kwa ajili ya Kituo cha Afya cha Iramba katika Jimbo langu la Serengeti na hali ya afya kule ni mbaya, ni kituo cha muda mrefu kimechakaa na kinahudumia watu wengi. Je, ni lini Serikali itapeleka tena hizo fedha milioni 400?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, hospitali ya Nyerere DDH inahudumia zaidi ya wakazi 100,000 katika Jimbo langu na idadi ya watumishi Saba iliyopelekwa bado kuna upungufu wa Madaktari 22, Wauguzi Wasaidizi 28 na Wauguzi wa kawaida 37.

Je, ni lini Serikali itatusaidia kuhakikisha tuna Madaktari wa kutosha na Wauguzi wengine?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jeremiah Mrimi Amsabi, Mbunge wa Jimbo la Serengeti kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali ilipeleka Shilingi Bilioni 2.36 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya Halmashauri ya Serengeti, kati ya fedha hizo, Shilingi Milioni 400 ilipelekwa kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha Iramba. Sasa kwa sababu Halmashauri walitumia fedha ile kujenga majengo ya hospitali ya Wilaya, kwanza naomba nitoe maelekezo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Serengeti kuhakikisha wanazingatia maelekezo ya Serikali. Fedha inapopelekwa kwa ajili ya kujenga vituo vya afya ijenge vituo vya afya kama ni zahanati ijenge zahanati, kama ni hospitali ijenge hospitali badala ya kuhamisha matumizi bila kibali maalum.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, natoa maelekezo katika mapato yao ndani watenge kwa awamu Shilingi Milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha Iramba.

Mheshimiwa Spika, kuhusina na Hospitali ya Nyerere DDH, ni kweli kwamba ina upungufu wa watumishi lakini Serikali imeendelea kupeleka watumishi, katika mwaka huu wafedha imetengewa ajira Saba kwa ajili ya kuonesha kwamba tunaendelea kupunguza upungufu wa watumishi katika hospitali hiyo. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. JEREMIAH M. AMSABI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kusaidia Hospitali ya Wilaya ya Serengeti na Nyerere DHH kwa kuzijengea uwezo wa kutoa huduma bora?

Supplementary Question 2

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Naomba kuuliza Serikali ni lini italeta fedha za awamu ya pili kuwezesha ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Ngara?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ndaisamba, Mbunge wa Jimbo la Ngara, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hospitali ya Wilaya ya Ngara ilipelekewa shilingi Milioni 500 mwaka wa fedha uliopita na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunajenga hospitali zetu hizi kwa awamu, sasa tunakwenda awamu ya pili ambapo katika mwaka wa fedha huu hospitali hii pia imetengewa Shilingi Milioni 500 na zitakwenda wakati wowote ndani ya mwaka huu wa fedha.

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JEREMIAH M. AMSABI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kusaidia Hospitali ya Wilaya ya Serengeti na Nyerere DHH kwa kuzijengea uwezo wa kutoa huduma bora?

Supplementary Question 3

MHE. LUCY J. SABU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa fursa hii ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka vifaa tiba ikiwemo mtambo wa kuzalisha oxygen katika hospitali ya Wilaya Meatu katika jengo la mahututi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Lucy John Sabu, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali katika mwaka huu wa fedha imetenga Shilingi Bilioni 69.95 kwa ajili ya kununua vifaa tiba na kuvipeleka katika vituo na hospitali zetu kote nchini. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwanza bajeti ya vifaatiba katika hospitali ya Wilaya ya Meatu tayari ipo, lakini tutakwenda kufanya tathmini kuona uwezekano wa kuwa na mtambo wa kuzalisha oxygen kulingana na mahitaji ili tuweze kuona namna ya kutekeleza wazo hilo.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JEREMIAH M. AMSABI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kusaidia Hospitali ya Wilaya ya Serengeti na Nyerere DHH kwa kuzijengea uwezo wa kutoa huduma bora?

Supplementary Question 4

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Hospitali ya DDH ya Ilula, bado inategemewa sana wananchi wa Tarafa ya Mazombe na Tarafa ya Mahenge. Je, Serikali ina mpango gani wa kuendelea kuipelekea fedha hospitali ili iweze kutoa huduma bora kama ilivyokuwa ikitoa mwanzo ilivyokuwa DDH kabla ya kujengwa hospitali ya Wilaya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Justine Nyamoga, Mbunge wa Jimbo la Kilolo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuhakikisha inawezesha hospitali zetu hizi za DDH kuendelea kutoa huduma kwa wananchi katika maeneo hayo. Kwanza kwa kuhakikisha kwamba fedha za mfuko wa pamoja health center basket fund zinaendelea kupelekwa, Hospitali hii ni moja ya hospitali zinazoendelea kupewa fedha hizo ili kuziwezesha kujiendesha na kutoa huduma bora, lakini pia kuangalia uwezekano wa kuendelea kuwapatia watumishi. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kuiunga mkono hospitali hii ili iendelee kutoa huduma kwa wananchi wa Mazombe na Tarafa zingine za karibu.