Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 68 2022-11-07

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. JEREMIAH M. AMSABI aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kusaidia Hospitali ya Wilaya ya Serengeti na Nyerere DHH kwa kuzijengea uwezo wa kutoa huduma bora?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jeremiah Mrimi Amsabi, Mbunge wa Jimbo la Serengeti, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kuanzia mwaka wa fedha 2017/2018 mpaka 2021/2022, imepeleka fedha Shilingi bilioni 2.36 kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kwa ajili ya kuboresha huduma zinazotolewa kwenye Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti. Fedha hizo zimetumika kujenga majengo saba (7) ya kutolea huduma ambapo majengo sita yamekamilika na yanatoa huduma na jengo moja la Wodi ya Mama na Mtoto lipo kwenye hatua ya ukamilishaji. Aidha, Serikali katika mwaka wa fedha 2021/2022, imepeleka katika hospitali hiyo watumishi 16 na vifaa na vifaatiba mbalimbali vya kutolea huduma za afya.

Mheshimiwa Spika, Hospitali Teule ya Nyerere (Nyerere DDH) katika mwaka wa fedha 2021/2022 imepokea vifaa tiba mbalimbali vya kutolea huduma za afya ikiwemo haematology machine, biochemistry machine na urine analyser. Aidha, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Hospitali hii imetengewa bajeti ya kuajiri watumishi saba (7) wa kada mbalimbali za afya.

Mheshimiwa Spika, ahsante.