Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: - Je, ni lini Wazee watapata nafasi ya uwakilishi Bungeni kama ilivyo kwa Vijana na Wanawake ili waweze kusikilizwa na kutoa ushauri?

Supplementary Question 1

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu aliyoyatoa Naibu Waziri, ukitazama Viti Maalum vina utaratibu maalum ambao umeshushwa na Tume mpaka kwenye vyama vya siasa. Je, haiwezekani sasa kuhakikisha kwamba utaratibu huu unashushwa ndani ya vyama vya siasa ili vyama hivi viwajibike kuwateua wazee ili na wenyewe waweze kupata nafasi ndani ya Bunge?

SPIKA: Mheshimiwa Conchester Rwamlaza hebu tusaidie, hilo kundi la wazee, unataka kundi la wazee kwa ujumla au kundi la wazee wanawake?

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Spika, kundi la wazee kwa ujumla wao bila kujali wanawake au wanaume.

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PATROBAS P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Conchesta Leonce Rwamlaza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Katiba yetu imeainisha vizuri katika vifungu hivyo, lakini pia ipo katika kifungu cha 36, 37 na 61 ambavyo vinatoa haki ya uwakilishi, lakini pia Ibara ya 21 ya Katiba, nayo pia inatoa haki ya kushiriki kwenye majukumu moja kwa moja ama kupitia uwakilishi. Zaidi kwenye Ibara ya 3 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inaeleza Tanzania ni Nchi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi ya kidemokrasia, kijamaa isiyofungamana na dini au isiyofuata misingi ya dini na ina mfumo wa vyama vingi vya siasa.

Mheshimiwa Spika, sasa katika vyama vingi vya siasa kwa mujibu wa sheria ya mwaka 1992, vyama vya siasa vinapewa haki ya kupata wawakilishi kwenye vyombo mbalimbali vya maamuzi, ikiwemo vyama hivi vya upinzani. Kwa mfano mzuri tu ambapo moja ya chama ambacho kinafanya hapa nchini vizuri kuna jumuiya ya vyama ambazo zinakuwa na wawakilishi wake, kuna moja ya chama kina umoja wa vijana UVCCM, lakini pili chama hicho kinao umoja wa wanawake, lakini pia kuna umoja wa wazazi na wawakilishi hao wote wameendelea kuwemo humo.

Mheshimiwa Spika, pengine hata Mheshimiwa naye atanikubalia, naye ni mmoja wa wawakilishi katika chama chake kwa sababu ni bibi yangu na ni mama, Mheshimiwa Conchester, kwa hiyo, nafasi hiyo inatolewa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.