Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 6 Policy, Coordination and Parliamentary Affairs Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 66 2022-11-07

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA aliuliza: -

Je, ni lini Wazee watapata nafasi ya uwakilishi Bungeni kama ilivyo kwa Vijana na Wanawake ili waweze kusikilizwa na kutoa ushauri?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PATROBAS P KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Conchesta Leonce Rwamlaza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Ibara ya 66(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, imeweka sharti la aina sita za Wabunge ambao ni Wabunge wa kuchaguliwa kuwakilisha Majimbo ya Uchaguzi, Wabunge Wanawake wasiopungua asilimia thelathini ya Wabunge wote, Wabunge watano kutoka Baraza la Wawakilishi, Mwanasheria Mkuu pamoja na Wabunge wasiozidi 10 wa kuteuliwa na Rais na Spika iwapo hatakuwa amechaguliwa kutoka miongoni mwa Wabunge.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Ibara ya 67(1)(b) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeainisha moja ya sifa ya mtu kuwa Mbunge ni lazima awe mwanachama na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa. Hivyo tunatoa wito kwa Vyama vya Siasa nchini kutenga nafasi za uwakilishi wa wazee kama ilivyo kwa watu wenye ulemavu na vijana ili waweze kupata nafasi ya uwakilishi Bungeni.