Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX K.n.y. MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Mradi wa Maji Kata ya Kazuramimba?

Supplementary Question 1

MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; je, ni lini Serikali itapeleka miradi ya maji katika Vijiji vya Lusawa, Mdoha, Ukuba na Janda katika Jimbo la Buhigwe?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Serikali ina mpango gani wa kutumia maji ya Mto Malagarasi kutatua changamoto ya maji katika Mkoa wa Kigoma? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nitumie nafasi hii kumshukuru Mheshimiwa Rais, mkakati wa Wizara yetu ya Maji hasa maeneo ya vijijini kuhakikisha kwamba itakapofika 2025 asilimia 85 ya upatikanaji wa maji iweze kutekelezeka. Tumeshapokea mitambo 25 na kila mkoa utakuwa na mtambo wake. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge maeneo yale ambayo ameyaainisha tutawapa kipaumbele ili kuhakikisha kwamba tunajenga miradi hii kwa wakati na wananchi waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Spika, eneo la pili, Mheshimiwa Rais ametupa maelekezo mahususi Wizara yetu ya Maji kwamba tutumie rasilimali toshelevu ikiwemo mito pamoja na maziwa ili kuhakikisha kwamba tunatatua changamoto kwa eneo kubwa sana. Kwa hiyo kikubwa nimhakikishie Wizara yetu ya Maji kwa eneo la Kigoma tumelenga kutumia Ziwa Tanganyika na Mto Malagarasi ili kuhakikisha kwamba tunakwenda kutatua changamoto hii ya maji.

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX K.n.y. MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha Mradi wa Maji Kata ya Kazuramimba?

Supplementary Question 2

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniona. Mradi wa Igongwi ambao unahudumia Kata tatu Matola, Luponde na Uwemba tunashukuru Serikali kwa pale tulipofikia, lakini unasuasua sana. Mheshimiwa Waziri anatoa kauli gani kwa wananchi wa Njombe kuhusiana na mradi huo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, nikushukuru. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, natambua mradi ule ni wa kimkakati ambao utatoa huduma kwa watu wengi sana. Mwezi huu tumekwishapokea zile fedha na moja ya maeneo ambayo tunatakiwa tulipe ni mradi ule. Nataka nimhakikishie mwezi huu tutalipa mradi ule wa maji.