Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 4 Water and Irrigation Wizara ya Maji 65 2022-11-04

Name

Nashon William Bidyanguze

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. KAVEJURU E. FELIX K.n.y. MHE. NASHON W. BIDYANGUZE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha Mradi wa Maji Kata ya Kazuramimba?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nashon William Bidyanguze, Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutekeleza Mradi wa Maji wa Kata ya Kazuramimba ambapo utekelezaji wake umefikia asilimia 90. Kazi zilizofanyika ni pamoja na ulazaji wa bomba kuu kilometa 3.3, ulazaji wa mabomba ya usambazaji Kilometa 26.7 na ujenzi wa tanki la ukubwa wa lita 470,000. Ujenzi wa mradi unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Novemba, 2022.