Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE K.n.y. MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, ni wananchi wangapi wameathirika na uvamizi wa wanyama wakali katika Wilaya ya Kyerwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; pamoja na uharibifu huo uliojitokeza wananchi hawa walihamishwa kwenye vitongoji vile kwa sababu ya uharibifu wa wale tembo. Mpaka sasa hivi wananchi wale wanaendelea kupata shida hakuna walicholipwa. Je, ni nini mpango wa Serikali angalau wa kuwapa fidia hawa wananchi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwenye Kata ya Businde, Kata ya Bugara pamoja Kikwechenkura, tembo wanaendelea kufanya uharibifu mkubwa, taarifa zinaendelea kutolewa lakini hakuna chochote ambacho Serikali inafanya. Je, ni nini mpango wa Serikali wa kudumu kuweza kuwahamisha wanyama hao waharibifu?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa
Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote nitoe pole kwa wananchi wote ambao wamekuwa wakikutwa na kadhia hii ya changamoto ya wanyama wakali na waharibifu. Serikali inatambua changamoto hizi na ndio maana tumeanza ujenzi wa vituo vya askari ili kusogeza huduma hii kwa ukaribu zaidi na wananchi waweze kutoa changamoto zao na huduma hii iweze kutolewa kwa haraka zaidi.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo tumeanza kufundisha vijana kwenye maeneo husika hususan vijana wa kwenye maeneo ya vijijini kama VGS ambao watashirikiana na askari kuhakikisha kwamba, wanyama wanaposogea katika maeneo ya shughuli za kibinadamu, basi iwe rahisi kuwaondoa.

Mheshimiwa Spika, nimwahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inachukua hatua na suala la kifuta machozi na kifuta jasho, tayari tumeshaanza kufanya tathmini na utekelezaji wake utafanyika hivi punde. Ahsante.

Name

Conchesta Leonce Rwamlaza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE K.n.y. MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, ni wananchi wangapi wameathirika na uvamizi wa wanyama wakali katika Wilaya ya Kyerwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita?

Supplementary Question 2

CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Wananchi 71 wa Kata ya Busindi, Kijiji cha Businde na Kitongoji cha Nyakabumbwe, pia katika Kijiji cha Nyakashenye, waliambiwa wapishe eneo lao kwa sababu ni ushoroba wa kupita tembo na waliahidiwa kupewa maeneo mengine, lakini hadi sasa pamoja na kupita katika mamlaka mbalimbali hawajapewa mahali popote. Je, ni lini Serikali itawapatia eneo la kuishi?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kuna maeneo ambayo yamevamiwa na shughuli za kibinadamu ikiwemo hata ujenzi wa nyumba. Eneo la Kitengule ni eneo ambalo ni ranch ambapo sasa wananchi walipoyavamia yale maeneo tembo wakawa kama wako kwenye kisiwa. Moja ya tiba ambayo tulitaka kuifanya ni kufungua ule ushoroba ili tembo waweze kuruhusiwa ku-move kwenda kwenye Hifadhi ya Burigi Chato. Tulielimisha wananchi katika eneo hilo na utaratibu sasa wa kufungua hizi shoroba ni pamoja na wananchi kukubali kupisha zile shoroba.

Mheshimiwa Spika, tunafanya tathmini na tukishafikia muda ambao ni muafaka fedha na namna ya kuwahamisha wale tembo basi tutarudi kwa wananchi kuwafahamisha zoezi hili. Ahsante.