Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 4 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 62 2022-11-04

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE K.n.y. MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: -

Je, ni wananchi wangapi wameathirika na uvamizi wa wanyama wakali katika Wilaya ya Kyerwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anatropia Lwehikila Theonest, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha miaka mitano, Wizara imepokea taarifa ya matukio ya wanyamapori wakali na waharibifu kutoka katika Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa ambapo jumla ya wananchi 54 katika Vijiji vya Kibare, Businde na Nyakashenyi walipata madhara ya uharibifu wa mazao yao uliosababishwa na tembo.