Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa Mahakama ya Mwanzo Chala?

Supplementary Question 1

MHE. VINCENT P. MBOGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nina swali moja la nyongeza. Jimbo la Nkasi Kusini Tarara ya Kate, huduma za kimahakama wanatumia godown; upande mmoja magunia, upande mmoja Mahakama inaendelea.

Mheshimiwa Spika, nilimpigia simu Mheshimiwa Naibu Waziri, akafika, tukatembelea Tarafa ya Kate yeye mwenyewe akajionea mazingira magumu, jinsi gani huduma za haki za kimahakama zinatolewa katika mazingira ambayo siyo mazuri. Ni godown, wakiweka dawa kwenye mazao, Mahakama haikaliki, ni harufu tupu: Je, ni lini serikali inakuja kujenga jengo la kisasa Tarafa ya Kate? Ahsante. (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa
Spika, ahsante sana. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vincent Mbogo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa sababu amekuwa akifuatilia sana masuala haya kwa ajili ya kuwasaidia wananchi kupata eneo sahihi la kupata huduma za haki. Ni kweli kabisa nilitembelea Kate, na nilikuta ni kweli wanatumia godown ambalo ndiyo linakuwa kama Mahakama.

Mheshimiwa Spika, vile vile nilimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba hili jambo tumelichukua na kwa sasa hivi katika ule mpango kazi ambao Mahakama imejiwekea, tunamwahidi Mheshimiwa Mbunge, katika kipindi hiki tunachoendelea nacho mpaka kufika 2025, Makao Makuu yote ya Tarafa nchini tunakwenda kujenga majengo ya Mahakama ya Mwanzo. Kwa hiyo, kwa sababu Kate ni Tarafa, inaenda kupata upendeleo wa pekee katika kipindi kijacho cha fedha. Ahsante. (Makofi)