Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaainisha bei rasmi za kuunganisha umeme maeneo ya kata za mjini zenye sura za vijiji?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Naishukuru Serikali kwa sababu wakati natoa swali hili nilikuwa na mahitaji ya kata mbili zenye mitaa zaidi ya 14, yenye sura za vijiji. Sasa hivi ninavyozungumza Kata za Lwanima na Kishiri, mkandarasi wa REA, kwa gharama ile ile ya Shilingi 27,000/= anaendelea kufanya kazi na wananchi wangu wanafurahia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naishukuru sana Serikali. Nitoe tu msisitizo uchambuzi huo utakapokamilika utatusaidia kujaziliza maeneo ambayo yatakuwa yamebaki kwa gharama nafuu kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kupokea pongezi na maombi ya Mheshimiwa Stanslaus Shing’oma Mabula, Mbunge wa yamagana na kwamba tunashukuru ameona Serikali inavyojitahidi kuendelea kutekeleza huduma hii ya kupeleka umeme kwa wananchi kwa gharama nafuu.

Mheshimiwa Spika, hili la kukamilisha zoezi la utambuzi wa maeneo kama tulivyojibu kwenye swali la msingi, tutahakikisha linakamilika kwa wakati na liweze kutusaidia katika maeneo yetu sote.

Mheshimiwa Spika, nami Jimbo langu la Bukoba Mjini likiwemo linafanana na la kwake pia.

Mheshimiwa Spika, nashukuru.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaainisha bei rasmi za kuunganisha umeme maeneo ya kata za mjini zenye sura za vijiji?

Supplementary Question 2

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Naomba tu nimwulize Mheshimiwa Naibu Waziri; tulileta malalamiko kuhusu hii miji midogo ambayo ina sura ya vijiji, mkasema tathmini inafanyika na hiyo timu itakuja kwa Wabunge ili tufahamu kama mnafika maeneo yetu. Sasa ni lini hii timu yenu itafika kwa Wabunge hawa? Ahsante.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Olelekaita, Mbunge wa Kiteto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli, tuliahidi kwamba kuna timu itaenda kuwatembelea na kuzungumza na Wabunge ili kuweza kubaini yale maeneo ambayo tunataka kuyafanyia kazi. Timu hii imeanza kufanya kazi ya ndani, ni kama ku-plot maeneo ambayo inatakiwa iende kuyatembelea kwa sababu kuna mengine yanafahamika, hayahitaji kwenda kukaguliwa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hii shughuli ya ndani ya utambuzi itakapokuwa imekamilika kwa taarifa iliyokuwepo, ndiyo sasa itaenda site na Waheshimiwa Wabunge wote wanaohusika wataiona hii timu kwa sababu maelekezo ya Wizara ndivyo yalivyo kwa ajili ya kushirikiana kuweza kutambua maeneo hayo kwa usahihi zaidi. Ahsante sana.