Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 60 2022-11-04

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaainisha bei rasmi za kuunganisha umeme maeneo ya kata za mjini zenye sura za vijiji?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Shing’oma Mabula, Mbunge wa Nyamagana, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na zoezi la utambuzi wa maeneo na wananchi wanaoishi katika maeneo ya Kata za Mjini zenye sura za vijiji.

Mheshimiwa Spika, zoezi hili linatarajiwa kukamilika mnamo mwezi Desemba, 2022 na baada ya zoezi hili Serikali itapanga bei muafaka za kuunganisha umeme kulingana na uhalisia wa maeneo husika.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.