Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanzisha Vituo vya Polisi katika Tarafa za Gonja na Mamba/Vunta?

Supplementary Question 1

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Tarafa ya Ulyankulu yenye kata saba haina kabisa Kituo cha Polisi, hali ambayo inapelekea vitendo vya kihalifu kuwa ni vingi: Je, ni lini Serikali itatujengea Kituo cha Polisi kwenye hii Tarafa ya Ulyankulu?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Rehema Migilla kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Tarafa ya Ulyankulu haina Kituo cha Polisi chenye hadhi ya tarafa, lakini ni suala la kuweka katika mipango yetu ili kiweze kufikiriwa kujengewa Kituo cha Polisi. Kwa hiyo, bajeti itakaporuhusu tutaliingiza hili na kituo kitajengwa kwenye hiyo Tarafa ya Ulyankulu.

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana.

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanzisha Vituo vya Polisi katika Tarafa za Gonja na Mamba/Vunta?

Supplementary Question 2

MHE. USSI SALUM PONDEZA: Mheshimiwa Spika, nami nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Nilikuwa nataka tu nami nipate majibu ya Mheshimiwa Waziri ya swali langu dogo la nyongeza. Nimekuwa nikiahidiwa mara nyingi sana, zaidi ya mara sita, saba juu ya vituo vyangu katika Jimbo langu la Chumbuni, lakini sijapata mwendelezo wala kujengewa vituo hivi na hali ya kiusalama kila siku zikivyoenda imekuwa siyo nzuri na wananchi wanafuata huduma mbali kiasi ambacho kama kuna mhujumu ametokea, basi watu kupata usaidizi inachukua muda mrefu sana.

Mheshimiwa Spika, nilikuwa naomba majibu ambayo yataeleza ni lini tutapata huduma hii katika Jimbo letu la Chumbuni?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ussi Pondeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Ussi anafahamu nilitembelea Zanzibar na kwenye jimbo lake nilifika nikaona hali ya vituo vidogo vya polisi vilivyopo na kwa kweli kwenye eneo lake anastahili kujengewa Kituo cha Polisi.

Mheshimiwa Spika, naomba tu upande wa Kamisheni ya Polisi ya Zanzibar iingize mahitaji ya Kituo cha Polisi eneo la Chumbuni ili iweze kupangiwa bajeti kwa ajili ya kuanza kujengwa kwenye bajeti itakayofuata.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.