Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 4 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 59 2022-11-04

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanzisha Vituo vya Polisi katika Tarafa za Gonja na Mamba/Vunta?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuwa na vituo vya Polisi katika maeneo mbalimbali nchini. Katika Tarafa ya Gonja kuna Kituo cha Polisi cha Daraja B kinachoongozwa na Mrakibu Msaidizi wa Polisi na kina Askari 16 na gari moja. Tarafa ya Mamba haina Kituo cha Polisi wala haijatenga eneo kwa ajili ya ujenzi wa kituo na makazi ya Askari. Hivyo tarafa, hiyo hupata huduma za Polisi toka kituo cha Polisi Gonja na vituo vidogo vya Polisi vya Kihurio na Ndungu vilivyo katika Tarafa ya Mamba.

Mheshimiwa Spika, ni ushauri wetu kwa Mheshimiwa Mbunge kushirikisha Halmashauri ya Wilaya ya Same kutenga eneo katika Tarafa ya Mamba kwa ajili ya kujenga Kituo cha Polisi, pamoja na nyumba za makazi ya Askari ili Serikali iweze kuingiza katika mpango wa kukitengea bajeti ya ujenzi.

Mheshimiwa Spika, nashukuru.