Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Barabara ya Sengerema – Nyamazugo – Nyehunge na Nkome kwa kiwango cha lami ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wakati wa Kampeni?

Supplementary Question 1

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu ya Serikali. Nataka niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwanza nashukuru sana Serikali kutuletea barabara ya lami, lakini ilishafanyika tathmini lakini wananchi wanasubiri malipo. Kwa sababu mchakato unaendelea, je tathmini italipwa lini?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa sababu barabara hii inahusisha Majimbo mawili, Jimbo la Sengerema na Jimbo la Buchosa, je Serikali iko tayari kuchukua ushauri wa wananchi wa Buchosa, kwamba ujenzi wa barabara hii uanzie Buchosa kuelekea
Sengerema badala ya Sengerema kuelekea Buchosa?
(Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Eric Shigongo, Mbunge wa Buchosa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilimuelewa kuhusu tathmini, nadhani ni fidia, italipwa lini? Kama nilimuelewa ni kwamba fedha ambazo tumetenga, kitu cha kwanza itakuwa ni kulipa fidia ya wananchi ambao watapisha ujenzi huo, halafu barabara itaanza kujengwa. Kwa hiyo, itakuwa ni hatua ya kwanza ya kufanywa kabla ya kuanza ujenzi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu ushauri alioutoa, kwa mujibu wa barabara ilivyo ni Sengerema-Nyamazugo- Nyehunge; hili suala ambalo tayari hata zabuni kama zimeshatangazwa, maana yake zinataja kuanzia wapi kwenda wapi. Kwa hiyo, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, pamoja na kwamba majimbo ni hayo mawili lakini barabara itaanzia huku tulikoitaja na kwenda pale inapokwisha kwa sasa. Ahsante sana.

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Barabara ya Sengerema – Nyamazugo – Nyehunge na Nkome kwa kiwango cha lami ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wakati wa Kampeni?

Supplementary Question 2

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Ninapenda kutaka kujua jibu la uhakika leo, ni lini barabara ya kutoka Kolandoto-Kishapu-Lalagwa hadi Meatu itajengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza la Mheshimiwa Minza, Mbunge wa Viti Maalum Simiyu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tumetenga fedha kuanza ujenzi wa Kolandoto hadi Lalago, bababara hii ambayo ni barabara kuu na tutaanza kwa kilometa 10 kwa sababu fedha tumetenga katika bajeti hii.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Barabara ya Sengerema – Nyamazugo – Nyehunge na Nkome kwa kiwango cha lami ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wakati wa Kampeni?

Supplementary Question 3

MHE. ATHUMANI A. MAIGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kuniruhusu na mimi niulize swali la nyongeza. Barabara ya Tabora - Mambali ambayo ufanisi wake umekwishafanyika siku nyingi, lini itaanzwa kujengwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maige, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Tabora - Mambali tulishakamilisha usanifu wa kina na fedha tumetenga; na Serikali inaendelea kutafuta fedha kuijenga hii barabara yote kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Barabara ya Sengerema – Nyamazugo – Nyehunge na Nkome kwa kiwango cha lami ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wakati wa Kampeni?

Supplementary Question 4

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Ipo ahadi ya kujenga kwa kilometa kumi kumi barabara kutoka Lushoto mpaka Mlalo. Je ni lini ahadi hiyo itaanza kutekelezwa? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli ahadi ilishatolewa na Serikali inatafuta fedha ili kuanza ujenzi wa hiyo barabara kwa kilometa kumi kwa kiwango cha lami. Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami, tumeshaanza, tumeshafika Magamba tukiwa tunaelekea Mlalo. Ahsante.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Barabara ya Sengerema – Nyamazugo – Nyehunge na Nkome kwa kiwango cha lami ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wakati wa Kampeni?

Supplementary Question 5

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi. Barabara ya Zamahero-Babayo- Makorongo hadi Donsee ndicho kipande pekee yake kitakuwa sasa hakina lami, ukizingatia barabara ya Kibarashi - Handeni hadi Singida inajengwa na ni kibarabara cha kilometa 18 tu, nataka kujua Serikali mna mpango gani wa kutumalizia hiko kibarabara?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Monni Mbunge wa Chemba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, alichosema ni kweli, barabara hii tutaijenga kwa kiwango cha lami lakini itategemea na upatikanaji wa bajeti. Kwa hiyo, Serikali inalifahamu na inaendelea kutafuta fedha ili kukamilisha hicho kipande ambacho ndicho kilichobaki. Ahsante.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Barabara ya Sengerema – Nyamazugo – Nyehunge na Nkome kwa kiwango cha lami ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wakati wa Kampeni?

Supplementary Question 6

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ambayo ipo kwenye ilani na ipo kwenye mpango wa maendeleo, kutoka Mtwara - Pachani - Rusewa na Rasi-Tunduru barabara hiyo ambayo ni barabara ya ulinzi, na Naibu Waziri uliitembelea na kuona umuhimu wa barabara hiyo ambayo ina viijiji visivyopungua 40?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli alichosema, barabara hii tumeitembelea na ni barabara muhimu ina kilometa zisizopiungua 300. Tumeshakamilisha usanifu wa kina na kabla ya kuanza tumeainisha maeneo yote korofi kwanza na madaraja ili tuweze kuyajenga wakati Serikali inaendelea kutafuta fedha kuijenga barabara yote hii muhimu kwa kiwango cha lami. Ahsante.