Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 4 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 57 2022-11-04

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Barabara ya Sengerema – Nyamazugo – Nyehunge na Nkome kwa kiwango cha lami ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wakati wa Kampeni?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, ninapenda kujibu Swali la Mheshimiwa Erick James Shigongo, Mbunge wa Buchosa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) ipo katika hatua za Manunuzi ya kumpata Mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa Barabara ya Sengerema – Nyamazugo – Nyehunge yenye urefu wa kilometa 54.4. Zabuni zilifunguliwa mnamo tarehe 30 Agosti, 2022. Uchambuzi wa zabuni unaendelea na mkataba wa kazi za ujenzi unatarajiwa kuwa umesainiwa ifikapo mwishoni mwa mwezi Novemba, 2022.