Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaendelea na matengenezo ya upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma uliosimama kwa muda wa mwaka mzima?

Supplementary Question 1

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, hivi karibuni kwenye ziara ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kigoma, Wizara ya Ujenzi imetoa taarifa kwamba mna mpango wa kuupanua uwanja huo running way yake kutoka 1.8 kilometa na kuja kilometa 3.1; na wananchi wamepata taarifa hizo, lakini mpaka sasa hawajui ni eneo gani mtalichukua la wananchi.

Je, ni lini Wizara yako itakwenda ku-earmark maeneo ambayo yatayachukua, ili maeneo ambayo hamyachukui wananchi waendelee na shughuli zao za maendeleo?

Je, baada ya kuyachukuwa, mtaweza kulipa fidia kwa wakati tofauti na ilivyokuwa hapo nyuma?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kilumbe Shabani Ng’enda, Mbunge wa Kigoma Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli ahadi imeshatolewa, lakini pia nataka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari hata usanifu Wizara imeshafanya tayari, kutoka kilometa 1.8 mpaka kilometa 3.1. Kuhusu fidia, tayari taratibu zinaendelea ili mara taratibu, na hasa tunataka uwanja utakapoanzwa kujengwa kwa awamu ya kwanza kwa uwekezaji wa fedha ndipo awamu ya pili itakapoanza kupanua uwanja.

Kwa hiyo nikuhakaikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tuanahitaji sana huo uwanja kuwa mrefu ili kupokea ndege. Serikali imejipanga kulipa fidia kwa wakati na kuanza kujenga, na taratibu zitakapoanza tutakuja kuwajulisha wananchi, wapi uwanja huo utapita. Ahsante.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaendelea na matengenezo ya upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma uliosimama kwa muda wa mwaka mzima?

Supplementary Question 2

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Kwa kuwa Serikali iliweka mpango wa kujenga viwanja katika mikoa kumi na moja, ukiwemo Mkoa wa Singida. Sasa nataka kujua ni lini ujenzi huu wa Uwanja wa Ndege Mkoa wa Singida utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Singida Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli mpango upo wa kujenga Uwanja wa Singida na kwa sasa Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kuanza kufanya feasibility study ya Uwanja wa Singida. Ahsante.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaendelea na matengenezo ya upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma uliosimama kwa muda wa mwaka mzima?

Supplementary Question 3

MHE. BUPE N. MWAKANG’TA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali.

Je, ni lini uwanja wa ndege wa Sumbawanga Mjini utaanza kujengwa? Nataka commitement ya Serikali.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Bupe Mwakang’ta, Mbunge wa Rukwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika jibu langu la msingi nililotoa, jibu hili linafanana kabisa na swali la Mheshimiwa Bupe. Tuna viwanja vinne ambavyo ni Kigoma, Sumbawanga, Tabora na Shinyanga, ambavyo vyote vinafadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Ulaya. Pia, huyu mfadhili ameshatoa fedha na muda wowote uwanja huu, kama nilivosema wa Kigoma, nao utaanza kujengwa ikiwa ni pamoja na Uwanja wa Tabora na Shinyanga. Ahsante.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaendelea na matengenezo ya upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma uliosimama kwa muda wa mwaka mzima?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Uwanja wetu wa Iringa ni uwanja ambao tayari umeshawekwa jiwe la msingi na Mheshimiwa Rais;

Je, ni lini sasa utakamilika kwa sababu ujenzi umechukuwa muda mrefu sana? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Iringa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, uwanja huu unaendelea kujengwa lakini pia uwanja huu World Bank imekubali kuufadhili, na kwa kuwa unaendelea. Kama kulikuwa na changamoto za kuchelewa, nataka nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kasi imeongezeka na tuna hakika uwanja utakamlishwa kwa sababu mkandarasi yupo site na anaendelea na kazi. Ahsante.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaendelea na matengenezo ya upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma uliosimama kwa muda wa mwaka mzima?

Supplementary Question 5

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Mkoa wa Simiyu upo kwenye ilani na eneo tayari limeshatengwa,

Je ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Uwanja wa Ndege Mkoa wa Simiyu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Simiyu, kama, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Uwanja wa Simiyu unatakiwa Kujengwa na mwaka huu tumetenga fedha kwa ajili ya kufanyia usanifu. Ahsante

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaendelea na matengenezo ya upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma uliosimama kwa muda wa mwaka mzima?

Supplementary Question 6

MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Lindi sasa hivi kuna gesi ambayo tunategemea itakuwa inawekezwa pale.

Je ni lini Uwanja wa Ndege wa Lindi Mjini utatatengenezwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Pathan, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Lindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Uwanja wa Lindi upo kwenye mpango, na katika bajeti hii upo kwenye mpango wa kuanza taratibu za kuujenga. Ahsante.