Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 4 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 56 2022-11-04

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaendelea na matengenezo ya upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma uliosimama kwa muda wa mwaka mzima?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Kilumbe Shabani Ng’enda, Mbunge wa Kigoma Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kazi ya matengenezo ya Upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kigoma yatafanyika kwa ufadhili wa Benki ya Uwekezaji ya Ulaya (European Investment Bank – EIB) pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, matengenezo yalisimama kwa sababu Mfadhili alichelewa kutoa idhini ya kumpata Mkandarasi atakakayetekeleza kazi hizo. Kwa sasa, idhini (No Objection) imeshatolewa.

Mheshimiwa Spika, mfadhili wa mradi huu ameshatoa fedha kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa mradi huu. Kwa sasa rasimu ya Mkataba imepelekwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa ajili ya mapitio.

Meshimiwa Spika, mara baada ya taratibu za vetting kukamilika na Mkataba kusainiwa, utekelezaji wa kazi za matengenezo ya upanuzi wa mradi wa Kiwanja cha Ndege cha Kigoma utaanza. Ahsante.