Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga minara ya simu katika Kata za Jimbo la Ludewa pamoja na kuongeza nguvu kwa minara iliyopo iwe 4G?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Ninaomba tu kufahamu kwa kuwa nilishamwandikia barua na tumezungumza, ni lini sasa atakuja Ludewa ili aweze kupokea shukrani za wananchi wa Ludewa kwa Mheshimiwa Rais?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Joseph Kamonga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Sita ni sikivu na ombi la Mheshimiwa Mbunge tunalipokea na mimi nitaongoozana nae kwenda kuangalia changamoto za wananchi wa Ludewa. Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga minara ya simu katika Kata za Jimbo la Ludewa pamoja na kuongeza nguvu kwa minara iliyopo iwe 4G?

Supplementary Question 2

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Takribani wananchi Elfu Sita wa Kijiji cha Katurukira Kata ya Mkula na Kijiji cha Sururu Kata ya Signari hawana mawasiliano mazuri ya simu. Je ni lini Serikali itawasaidia wananchi miundombinu ili waweze kupata mawasiliano mazuri ya simu?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Kilombero kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mradi wa Tanzania ya Kidigitali (Digital Tanzania) na tayari mradi huu tenda yake imeshatangazwa tarehe 20 Oktoba na tarehe 2 Disemba tayari mradi utafunguliwa ambapo Kata na Vijiji vya Jimbo la Kilombero vimeingizwa katika mradi huo. Hivyo, Mheshimiwa Mbunge asiwe na wasiwasi pindi mchakato huu utakapokamilika basi ujenzi wa minara utaanza kufanyika rasmi katika Jimbo lake.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga minara ya simu katika Kata za Jimbo la Ludewa pamoja na kuongeza nguvu kwa minara iliyopo iwe 4G?

Supplementary Question 3

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Kata ya Lahoda iliyopo Wilaya ya Chemba ina mnara ambao hauna nguvu, hivyo kuleta shida katika mawasiliano. Je, ni nini mkakati wa Serikali katika kuhakikisha kwamba wanaimarisha mawasiliano ili wananchi wa Kata hii waweze kupata mawasiliano? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Fatma kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika Jimbo la Chemba tayari tumeshatuma wataalamu wetu kwenda kuangalia changamoto iliyopo katika minara katika Jimbo la Chemba. Kikubwa tulichokuwa tunakiangalia ni aidha kuangalia kama kulikuwa na huduma ya 4G au haikuwepo, lakini kama ilikuwepo na changamoto ni mawasiliano hafifu basi tutahakikisha kwamba tunafanya namna ya kuongeza nguvu katika minara hiyo inayo lalamikiwa na wananchi. Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga minara ya simu katika Kata za Jimbo la Ludewa pamoja na kuongeza nguvu kwa minara iliyopo iwe 4G?

Supplementary Question 4

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, ahsante, Serikali itapeleka lini mawasilino ya uhakika ya simu kwa wananchi wa Ushetu hasa katika Kata ya Ulewe, Igwamanoni, Igunda pamoja na Bukomela ambapo wananchi hao bado wanapanda juu ya mti na milimani kutafuta mawasiliano ambayo ni hatari sana kwenye maisha yao.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cherehani Mbunge wa Ushetu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kata ambazo Mheshimiwa Cherehani amezitaja tayari katika bajeti ya Serikali ambayo ililetwa Bungeni hapa Kata hizo ziliwekwa katika bajeti. Bajeti hii ambayo inaunganisha minara 763 na kama ambavyo nimesema hapo mwanzoni tayari tumeshatangaza tenda tarehe 20 Oktoba na tarehe 2 Disemba itafunguliwa na baada ya hapo ujenzi wa minara hii utaanza mara moja. Ahsante.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga minara ya simu katika Kata za Jimbo la Ludewa pamoja na kuongeza nguvu kwa minara iliyopo iwe 4G?

Supplementary Question 5

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Wakati wenzetu wanakwenda kwenye mfumo wa 4G Jimboni kwangu baadhi ya Vijiji havina kabisa mawasiliano ikiwepo Kijiji cha Mhanga, Kintanula na Kijiji cha Lulanga.

Je, ni lini sasa Serikali itatimiza ahadi yake ya muda mrefu ya kupeleka minara katika vijiji hivyo?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Masare kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge tunawasiliana mara kwa mara na hivi vijiji tayari kilichokuwa kinasubiriwa ni tenda kutangazwa na tenda tayari imeshatangazwa Tarehe 20 Oktoba. Hivyo, tunasubiri mchakato huu ukamilike ili utekelezaji wa mradi huu uanze mara moja. Mimi pamoja na Mheshimiwa Mbunge bahati nzuri tumeshafika katika eneo lake na vijiji ambavyo amevitaja mimi binafsi nimeshafika katika maeneo hayo, kwa hiyo nimhakikishie kwamba hilo ninalifahamu kabisa na Serikali itaenda kutekeleza. Ahsante sana.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga minara ya simu katika Kata za Jimbo la Ludewa pamoja na kuongeza nguvu kwa minara iliyopo iwe 4G?

Supplementary Question 6

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itajenga Minara ya simu katika Kata ya Makame na Raiseli katika jimbo la Kiteto?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asia Halanga, Mbunge Viti Maalum Manyara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kwelli kabisa kuna changamoto ya Mawasiliano katika jimbo la Kiteto. Na bahati nzuri Mheshimiwa Mbunge wa Kiteto, ndugu yangu wakili msomi Olelekaita pamoja na Mheshimiwa Asia, kwa kweli tunashirikiana vizuri sana na wao katika kuhakikisha tunatatua changamoto hii. Bahati nzuri Mheshimiwa Mbunge anafahamu kabisa kuwa orodha ya vijiji vyake vyote vipo kwenye bajeti ya mwaka huu. Hivyo niwaombe Waheshimiwa Wabunge wa Manyoni pamoja na Kiteto, tuhakikishe kwamba tunashirikiana katika kutoa maeneo ili kukamilisha ujenzi wa miradi hii. Ahsante sana.