Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 3 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 47 2022-11-03

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga minara ya simu katika Kata za Jimbo la Ludewa pamoja na kuongeza nguvu kwa minara iliyopo iwe 4G?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Zacharius kamonga Mbunge wa Ludewa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mpaka sasa Seriakili kupitia Mfuko wa mawasiliano kwa wote UCSAF inaendelea kutatua changamoto za mawasiliano katika Jimbo la Ludewa kwa kushirikiana na watoa huduma wa mawasiliano kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Airtel ambao sasa tayari imewasha minara mitatu katika Kata za Madiru Kijiji la Ilawa, Kata ya Madope Kijiji cha Lusitu na Kata ya Mkongobaki katika Kijiji cha Mkongobaki.

Mheshimiwa Spika, kampuni ya tiGo ambayo imejenga minara katika Kata ya Lupanga, Kijiji cha Lupanga, Kata ya Mkomang’ombe Kijiji cha Mkomang’ombe na Kata ya Ludewa Kitongoji cha Ngalahawe ambapo mnara unafika katika Kijiji cha Nindi. Aidha, kampuni ya simu ya tiGo ipo katika hatua za kutekeleza mradi wa kufikisha huduma ya mawasiliano katika Kata ya Lupingu na Mkwimbili ambapo changamoto kubwa imekuwa ni namna ya kusafirisha vifaa vya ujenzi wa mnara na kuvifikisha katika eneo la mradi.

Mheshimiwa Spika, pia Halotel inatoa huduma katika Kata zote za mwambao wa Ziwa Nyasa zikiwemo Makonde, Kimata, Nsele, Ndowa na Igalu. Hata hivyo, Serikali inatambua changamoto kubwa ya mawasiliano inayowakabili wananchi wote wa kandokando ya Ziwa hususa ni Tarafa ya Jua. Kwa upande mwingine, TTCL inatoa huduma katika Kata ya Ibumi japo bado kuna changamoto hasa katika Kijiji cha Masimalavafu. Serikali inatambua kuwa mradi wa uchimbaji wa madini ambao kwa namna moja au nyingine utachangia pato la uchumi kwa nchi yetu. Hivyo, Serikali kupitia mfuko wa mawasiliano kwa wote UCSAF inatumia wataalam wake kwenda kata ya Ibumi na kuangalia namna gani ya kutatua changamoto ya mawasiliano hususa ni katika eneo la uchimbaji wa madini.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na nguvu ya minara kwenda teknolojia ya 4G. Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote imeanza kutekeleza mradi wa kuongeza nguvu kwenye minara yote nchini iliyokuwa na teknolojia ya 2G kwenda 3G na 4G. Hivyo, minara iliyopo Jimbo la Ludewa itaingizwa katika mradi huo. Ahsante sana.