Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani juu ya mashamba makubwa yanayomilikiwa na wawekezaji na hayatumiki kuzalisha mali na ajira nchini?

Supplementary Question 1

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ili kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Namshukuru Mheshimiwa naibu kwa Majibu yake mazuri.

Mheshimiwa Spika, naomba kutaka kujua, kwa kuwa watu wa Aga Khan kwa maana ya Taasisi ya Aga Khan wanasema kwamba ninyi Wizara ya Ardhi pamoja na Wizara nyingine Tano ikiwemo Mambo ya Nje, Mambo ya Ndani, mnazuia wao wasiendeleze shamba hilo kwa kuwa kuna jambo ambalo hamkulifanya ili waweze kuendeleza shamba hilo. Nini kauli ya Serikali kuhusu taasisi hiyo?

Swali la pili, ni lini utatembelea shamba hilo ili kujua wazi dhahiri shahiri kwamba kuna nini juu ya jambo hilo? Ahsante.

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO
YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nitoe taarifa kuhusu shamba hili la Aga Khan. Shamba hili wakati linaombwa mwanzo liliombwa kwa ajili ya kilimo, lakini kutokana na maendeleo ya ukuaji wa Mji wa Arumeru Magharibi ikalazimika matumizi ya shamba lile yabadilike na kuwa eneo la kupanga Mji kwa maendeleo ya maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hilo kumetokea changamoto baina ya maeneo ambayo yanaendelezwa na hii Taasisi ya Aga Khan na Serikali, hivyo ndivyo mgogoro anaouzungumza Mheshimiwa Mbunge ulipoibuka. Maelekezo ya Serikali ni kwamba, punde tutakapo maliza mazungumzo hayo taratibu nyingine kwa ajili ya uendelezaji zitaendelea.

SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, swali lake la pili ulikuwa umeshalijibu?

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, kwa upande wa ombi la kwenda kuona shamba hilo ili kuona maendeleo mengineyo. Natoa ahadi kwamba niko tayari kuongozana na Mheshimiwa Mbunge ili kuona na kufuatilia yanayoendelea katika shamba hilo.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani juu ya mashamba makubwa yanayomilikiwa na wawekezaji na hayatumiki kuzalisha mali na ajira nchini?

Supplementary Question 2

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza.

Kwa kuwa, ripoti ya sensa ya sasa ya mwaka 2022 imeonesha wazi kwamba ongezeko la watu ni zaidi ya Milioni 16 katika kipindi cha miaka Kumi, hii imeshabihiana sana na wananchi wengi wasio na ardhi kuvamia mapori yasiyo endelezwa kwa miaka mingi.

Je, Serikali haioni sasa kuna haja ya kufanya tathmini upya ili yale maeneo ambayo hayajaendelezwa na wananchi wako mle wamejenga waweze kurasimishwa rasmi?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, kwangu mimi na upande wa Serikali ninaamini ushauri uliotolewa na Mheshimiwa Mtemvu Mbunge ni jambo nzuri na ni jambo la kufanyiakazi nasi ndani ya Wizara nataka nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa tumekwishapokea taarifa ile ya sensa na ndani yake yako mambo mengi sana ikiwemo kuangalia jinsi gani Serikali sasa inaenda kuondokana na maeneo ambayo hayajapangwa vizuri lakini pia kurasimisha maeneo ambayo yameiva kwa ajili ya urasimishaji.

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani juu ya mashamba makubwa yanayomilikiwa na wawekezaji na hayatumiki kuzalisha mali na ajira nchini?

Supplementary Question 3

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa zaidi ya miaka Sita wananchi wa Korogwe wanalia na shamba la Mwakinyumbi lililotelekezwa na Serikali imekuwa ikituahidi lakini hakuna matokeo. Mheshimiwa Waziri ni nini sababu inayoifanya Serikali ishindwe kulifuta shamba la Mwakinyumbi na kuwarudishia wananchi wafanye shughuli za uzalishaji? (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Mnzava Mbunge wa Korogwe swali lake kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli juu ya shamba hilo ambalo limetajwa na Mheshimiwa Mbunge taarifa zimeshafika Wizarani na taratibu za kiutawala kwa ajili ya kulitwaa shamba hilo na kulirudisha kwa wananchi zinaendelea na tutakapo kuwa tayari tutakupa taarifa za kina juu ya jibu la maombi ya wananchi wa Korogwe.