Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 3 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 46 2022-11-03

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani juu ya mashamba makubwa yanayomilikiwa na wawekezaji na hayatumiki kuzalisha mali na ajira nchini?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Noah Lemburis Saputu, Mbunge wa Arumeru Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kuwa yapo mashamba makubwa nchini ambayo yamegawiwa kwa wawekezaji ambapo baadhi ya mashamba hayo yanatumika kwa uzalishaji mali na ajira na mengine hayatumiki kama ilivyokusudiwa. Wizara kwa kushirikiana na taasisi nyingine imeanza kushughulikia changamoto mbalimbali zinazowakabili wawekezaji kwa kufanya ukaguzi na kuainisha changamoto zilizopo.

Mheshimiwa Spika, hatua inayofuata ni kufanya majadiliano na wawekezaji waliobainika kuwa na changamoto ili kuzipatia ufumbuzi kwa pamoja kwa lengo la kuongeza tija katika uzalishaji. Kwa mashamba ambayo yametelekezwa, Wizara imeendelea kuchukua hatua za kisheria kwa wamiliki walioshindwa kutekeleza masharti ya uwekezaji ikiwemo kuyarudisha na kuyapangia matumizi upya kwa manufaa ya umma.