Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza: - Je, ni lini TFS itaanza kutoa vibali vya malisho kwa wafugaji kama inavyotoa vibali vya kuvuna mbao na mkaa ili Serikali ipate mapato?

Supplementary Question 1

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; ni kweli sheria inataka hivyo, lakini kwa kuwa shughuli za kibinadamu zinaendelea kama uvunaji wa mikaa na kuvuna miti katika misitu hiyo ya TFS, je, Serikali hawezi kuona sasa wakati umfefika wa ku-review sheria hiyo ili kwenda na wakati?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; tunaona hifadhi nyingi ambazo zinachomwa kwa makusudi katika utaratibu wa kuachia muda majani yaote. Je, Serikali haioni kwamba hata utaratibu huo pia umepitwa na wakati, wakati umefika sasa wa kuruhusu watu kuvuna majani ili kutoa suluhisho ya malisho ya ng’ombe ambao sasa hivi wanahangaika hasa katika maeneo ya wafugaji?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Innocent Kalogeris akiwakilishwa na Mheshimiwa Londo, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nijibu haya maswali mawili kwa pamoja kwamba ni kwa nini tunafanya usafi kwenye maeneo ya hifadhi hususani kuchoma majani na Mheshimiwa Mbunge amesema badala ya kuchoma hayo majani basi yangetumika kwa ajili ya mifugo. Kiutaalam wa kiuhifadhi, wanashauri endapo kuna na mahitaji ndani ya hifadhi, ikiwemo mbolea, lakini pia kuna calcium ambayo wanaitumia wanyama pori, basi huwa kuna maeneo ambayo yameainishwa ambayo yanatengeneza hiyo calcium kwa kuchomwa jivu, ili wanyamapori waweze kupata calcium waendelee ku- survival kwenye maeneo yao ya hifadhi.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo jivu hili huwa linatengeneza mbolea ili iweze kusaidia kuendelea kumea kwenye yale majani ambayo yanatumika kwa ajili ya malisho ya wanyamapori.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza: - Je, ni lini TFS itaanza kutoa vibali vya malisho kwa wafugaji kama inavyotoa vibali vya kuvuna mbao na mkaa ili Serikali ipate mapato?

Supplementary Question 2

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Kwanza naishukuru sana Serikali kwa namna ambayo kwa kweli wameweza kudhibiti moto uliokuwa unawaka ndani ya Mlima Kilimanjaro. Katika dhana hiyo hiyo ya kudhibiti, je, Serikali haioni iko haja ya kufanya mabadiliko ya sheria ili wananchi wanaozunguka Mlima Kilimanjaro waweze kupata service levy kama ilivyo kwenye maeneo mengine yenye mgodi ili kuongeza sense of ownership ya wananchi wanaozunguka kuona mlima ule ni mali yao? Ahsante.

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunapokea mawazo yake, lakini bado tunatambua kwamba wananchi wanaozunguka maeneo ya Mlima Kilimanjaro, ni sehemu ya hifadhi na mara nyingi tumekuwa tukihamasisha upandaji wa miti ili kulinda hifadhi hii ili iweze kutunzwa vizuri. Kwa hiyo, tunalipokea hili pia la sheria ili tuweze kuangalia utaratibu mwingine kuhakikisha mlima huu tunautunza vizuri.