Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 3 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 43 2022-11-03

Name

Innocent Edward Kalogeris

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO K.n.y. MHE. INNOCENT E. KALOGERIS aliuliza: -

Je, ni lini TFS itaanza kutoa vibali vya malisho kwa wafugaji kama inavyotoa vibali vya kuvuna mbao na mkaa ili Serikali ipate mapato?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Edward Kalogeris, Mbunge wa Morogoro Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Misitu, Sura ya 323, Kifungu cha 26(n) kinakataza kuingiza au kuchunga mifugo kwenye maeneo ya hifadhi. Aidha, Kanuni za Misitu za mwaka 2004, Kifungu cha 14(4) kimeweka katazo la kutoa vibali vya kuchunga au kulisha mifugo au kufanya shughuli za kilimo kwenye hifadhi za misitu.

Mheshimiwa Spika, ni dhahiri kuwa kuchunga, kulisha mifugo au kufanya shughuli za kilimo kwenye maeneo ya hifadhi za misitu ni kuvunja sheria. Hivyo, sheria zimewekwa ili kulinda rasilimali zilizomo hifadhini kwa matumizi endelevu ya rasilimali za misitu kwa kizazi cha sasa na vijavyo.