Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS K.n.y. MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza majengo katika Kituo cha Afya Itobo Wilayani Nzega?

Supplementary Question 1

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Ni kweli majengo yameshaanza kujengwa katika kituo cha Itobo pamoja na kuendeleza; Serikali imekuwa ikipeleka fedha na kujenga majengo nusu baadhi ya vituo, kikiwemo Kituo cha Igalula, jengo la OPD halijajengwa, Kituo cha Lutete majengo hayajakamilika: -

Je, nini mikakati ya Serikali kupeleka fedha kumalizia vituo vya afya vyote ili wananchi waendelee kupata huduma? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Venant Protas, Mbunge wa Jimbo la Igalula kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikijenga vituo vya afya kwa awamu kwa kupeleka fedha awamu ya kwanza kujenga majengo ya awali na awamu ya pili kumalizia majengo yaliyobaki.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge, kuna baadhi ya vituo vya afya vimepata awamu ya kwanza Shilingi milioni 250, vitapelekewa awamu ya pili Shilingi milioni 250 kutimiza Shilingi milioni 500. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba vituo vya afya ambavyo bado havijakamilishwa, fedha itapelekwa awamu ya pili ili kukamilisha majengo yale na vituo vianze kutoa huduma kwa wananchi. Ahsante sana.

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS K.n.y. MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza majengo katika Kituo cha Afya Itobo Wilayani Nzega?

Supplementary Question 2

MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Spika, nashukuru wa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wakati wa ziara ya Mheshimiwa Waziri Mkuu pale Kijiji cha Chomachankola, Tarafa ya Choma, Mheshimiwa Waziri Mkuu aliahidi kutupatia fedha kuongeza kwenye Kituo cha Afya cha Choma: -

Je, ni lini sasa Wizara italeta fedha kwa sababu ahadi hii imetolewa toka 2018? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Seif Gulamali, Mbunge wa Jimbo la Manonga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali iliahidi kupeleka fedha kwa ajili ya Kituo cha Afya cha Choma, Kijiji cha Chomachankola katika Jimbo la Manonga na ni kweli kwamba Mheshimiwa Mbunge amefuatilia kwa karibu sana, na mwaka wa fedha uliopita tulikosa kifungu cha kupelekea fedha ile, lakini nimeongea naye na tumekubaliana katika mwaka wa fedha huu tutahakikisha fedha inapelekwa ili kitu cha afya kianze kujengwa. Ahsante.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS K.n.y. MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza majengo katika Kituo cha Afya Itobo Wilayani Nzega?

Supplementary Question 3

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi. Mwaka 2008 Serikali ilianza ujenzi wa jengo la mama na mtoto kwenye zahanati ya Kijiji cha Msada, Kata ya Msada, lakini mpaka leo ni miaka 14 lipo kwenye renter. Naomba kujua ni lini sasa Serikali itatoa fedha za kumalizia?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mohamed Lujuo Monni, Mbunge wa Jimbo la Chemba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali iliweka utaratibu wa kutumia fedha kutoka Serikali Kuu na pia kutumia fedha kutoka mapato ya ndani halmashauri kukamilisha baadhi ya majengo na hususan majengo katika ngazi ya zahanati. Kwa hiyo, naomba nichukue fursa hii kumwelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba, kuhakikisha wanatenga fedha katika asilimia 40 ya miradi ya maendeleo kukamilisha jengo la mama na mtoto katika zahanati ambayo Mheshimiwa Mbunge ametaja. Ahsante.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS K.n.y. MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza majengo katika Kituo cha Afya Itobo Wilayani Nzega?

Supplementary Question 4

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipatia nafasi. Je, ni lini Serikali itaboresha kituo cha afya cha Ndalambo ikiwa ni sambamba na kuongeza majengo? Kituo hiki kinahudumia kata zaidi ya tano zilizopo kwenye Tarafa ya Ndalambo. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Condester Sichalwe, Mbunge wa Jimbo la Momba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya tathmini ya vituo vya afya ambavyo ujenzi wake ulianza, lakini haujakamilika na inaweka mpango wa kukamilisha vituo vya afya vile havijakamilika ili viweze kutoa huduma za afya kwa wananchi. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kuwa kituo kile kilishaanza ujenzi na hakijakamilika, tutakwenda kukamilisha kituo hicho.

Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii pia kutoa taarifa kwa Waheshimiwa Wabunge kwamba mpango na dhamira ya Serikali ni kukamilisha kwanza vituo vya afya ambavyo vilianza ujenzi na havijakamilika ili vipate vifaa tiba na kuanza kutoa huduma za afya kabla ya kuendelea kujenga vituo vingine vipya. Vile vile tutaendelea kujenga zahanati za kimkakati isipokuwa vituo vya afya vipya mpaka pale tutakapokuwa tumekamilisha ujenzi wa vituo vya vya afya ambavyo tayari vimeshaanza. Ahsante sana.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS K.n.y. MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza majengo katika Kituo cha Afya Itobo Wilayani Nzega?

Supplementary Question 5

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa Kata ya Mlowa, Kijiji cha Mkolango, wananchi wa Mkolango wamejenga zahanati pamoja na Diwani na Mbunge; na Rais alipokuja tulimweleza jambo hili na aliahidi kwamba sasa atakwenda kumalizia kwa sababu imekwisha, wameshaezeka na kila kitu; na Naibu Waziri na Waziri walikuwepo na ndiyo mlisikia: Sasa je, ni lini mtatuletea fedha ili wananchi wa Mkolango muweze kuwaunga mkono zahanati hii imaliziwe?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Sanga, Mbunge wa Jimbo la Makambako, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue fursa hii kuwapongeza wananchi wa Kata ya Mlowa, Kijiji hiki cha Mukolango kwa kutoa nguvu zao kwa kushirikiana na Mheshimiwa Mbunge kuanza ujenzi wa zahanati. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, katika bajeti ya Serikali ya mwaka huu wa fedha, fedha zimetengwa kwa ajili ya kukamilisha maboma ya zahanati na tutatoa kipaumbele katika zahanati hii ambayo Mheshimiwa Mbunge amesema. Ahsante.

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. VENANT D. PROTAS K.n.y. MHE. JACQUELINE K. ANDREA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza majengo katika Kituo cha Afya Itobo Wilayani Nzega?

Supplementary Question 6

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kituo cha Afya cha Changuge, Tarafa ya Gelango, Wilaya ya Rorya ni moja ya kituo ambacho kimejengwa muda mrefu sana na kwa sasa majengo yake yamechakaa na hata yaliyopo hayatoshelezi kulingana na mahitaji ya tarafa na kata ile. Nataka nijue mpango wa Serikali sasa kuboresha vituo vya afya vile vya zamani ili angalau viendane sasa na kasi na uhitaji wa wananchi wa sasa. Nini mpango wa Serikali katika kuboresha vituo vya afya vya zamani?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jafari Chege, Mbunge wa Jimbo la Rorya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba katika maeneo mbalimbali kote nchini kuna baadhi ya vituo vya afya na hospitali za halmashauri ambazo ni chakavu, na Serikali imeweka kanzidata kwa kutambua vituo vya afya chakavu na itaendelea kutenga fedha kwa awamu kwa ajili ya ukarabati wa vituo hivyo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba tuichukue hii hoja ya Mheshimiwa Mbunge, tufanye tathmini ya kituo hicho cha afya na kuona uwezekano wa kutafuta fedha kwa ajili ya kufanya matengenezo. Ahsante.