Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ahmed Ally Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Solwa

Primary Question

MHE. AHMED A. SALUM aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Mwanangwa – Mwakitolyo hadi Bulige Wilayani Kahama kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 2025?

Supplementary Question 1

MHE. AHMED A. SALUM: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza. Kwa kuwa barabara hii ni muhimu sana, inaunganisha wilaya tatu, kwa maana ya Kahama, Shinyanga pamoja na Misungwi, na kwa kuwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ni mazuri lakini kwa namna ambavyo wameanza, ni jambo jema sana na namshukuru sana kwa sababu hatua za awali zinaonesha kwamba barabara hii tayari imeanza kujengwa.

Mheshimiwa Spika, kama Serikali itaendelea kujenga kilometa 5.6, maana yake tutachukua zaidi ya miaka 20 kwenye ukamilishaji wake. Swali la kwanza; je, mwaka huu wa fedha kwanini Mheshimiwa Naibu Waziri, au Wizara hii isiongeze fedha angalau kilometa zaidi ya 20 au 30 ili barabara hii iweze kuonyesha mwelekeo wa kukamilika?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa barabara hii, ipo kwenye Ilani ya Uchaguzi wa 2015-2020 na 2020-2025, ilani ya chaguzi mbili na kwa kuwa barabara hii ni muhimu sana. Je, kwanini Serikali isiweke na kuonesha commitment kabisa ya moja kwa moja, ikatenga fedha kwenye ukamilishaji wa barabara hii, ikajengwa mpaka kukamilika kwake kabisa kabla ya mwaka 2025?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ahmed Ally Salim, Mbunge wa Solwa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge wa Solwa, kwa jinsi anavyofuatilia ujenzi wa barabara hii; na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunachokifanya ni kile ambacho tumekipata na fedha inayopatikana kwa kiasi chochote sisi tutaendelea kujenga, tunapunguza.

Mheshimiwa Spika, lengo la Serikali ni kuijenga barabara hii mihimu ambayo ni njia ya mkato kutoka Mwanza kwenda Kahama. Kama alivyoainisha, imeainishwa kwenye Ilani ya Uchaguzi. Tunaamini ndani ya mwaka huu, katika miaka inayokuja, barabara hii itatengewa fedha ili iweze kujengwa kwa kiwango cha lami kadri fedha itakavyopatikana. Ahsante sana.

Name

Festo Richard Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. AHMED A. SALUM aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Mwanangwa – Mwakitolyo hadi Bulige Wilayani Kahama kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 2025?

Supplementary Question 2

MHE. FESTO R. SANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Swalli langu dogo la nyongeza, barabara ya Makete-Mbeya-Isionji, ni barabara ambayo tayari upembuzi yakinifu, hatua za manunuzi, na hata upekuzi wa kampuni iliyoshinda umeshafanyika. Mheshimiwa Waziri mbele ya Mheshimiwa Rais alituahidi mwezi wa tisa mkandarasi atafika site.

Je, ni lini mkandarasi atasaini mkataba ili aanze kujenga barabara hii ambayo ni uti wa mgongo wa uchumi wa Wilaya ya Makete?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Festo Sanga, Mbunge wa Makete, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara anayoitaja Mheshimiwa Festo ilitangazwa, lakini ilikosa Mkandarasi kwa sababu ya udogo, Mheshimiwa Rais akaongeza kilomita. Barabara hii ilishatangazwa na tayari mikataba imeshaandaliwa. Tunapoongea sasa hivi iko kwa Mwanasheria Mkuu kwa ajili ya kuifanyia vetting na tunategemea mara itakapotoka mwezi huu, basi mikataba hiyo itasainiwa ili ianze kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante.