Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 2 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 36 2022-11-02

Name

Ahmed Ally Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Solwa

Primary Question

MHE. AHMED A. SALUM aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Mwanangwa – Mwakitolyo hadi Bulige Wilayani Kahama kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 2025?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ahmed Ally Salim, Mbunge wa Solwa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Mwanangwa – Mwakitolyo hadi Bulige yenye urefu wa kilomita 118.8 ni sehemu ya barabara itokayo Mwanangwa – Misasi - Salawe – Solwa - Kahama yenye urefu wa kilomita 148.8. Serikali tayari imeanza ujenzi kwa awamu ambapo kilomita 5.65 kuanzia Kahama kuelekea Solwa na sehemu ya mita 450 katika mji wa Bulige zimekamilika kwa kiwango cha lami. Katika mwaka wa fedha 2022/2023, kiasi cha Shilingi milioni 750.62 zimetengwa kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa kilometa 1.2. Ahsante.