Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia watoto wa mitaani ambapo kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa?

Supplementary Question 1

MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, watoto hawa wa mitaani ndio watoto ambao wanazalisha makundi kama panya road, damu chafu na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, katika majibu yake Mheshimiwa Waziri amesema kwamba Serikali inazo nyumba za kulelea hawa Watoto. Ningeomba kujua Serikali ina vituo vingaapi vya kulelea watoto wa mitaani.

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Nchi yetu ya Tanzania imesaini mikataba mbalimbali ya kimataifa kuhusu Watoto. Kwa mfano The UN Convention on the Right of the Child na mkataba wa Afrika wa The African Charter on the Right of the Child. Swali langu; je, Serikali inamkakati gani wa kuhakikisha kwamba watoto wa Tanzania ambao wako mitaani wanapata elimu ambayo ni haki yao pamoja na kujua haki zao za msingi?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA,WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Taska kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inavituo viwili vya kulea Watoto ambavyo inavimiliki. Vituo hivyo ni Kurasini ambacho kipo Dar es Salaam na Kikombo ambacho kipo Dodoma. Vituo hivyo vina idadi ya Watoto 142 ambapo 88 wakiwa ni wakiume na 54 ni wa kike.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, watoto wote ambao wanalelewa katika vituo vya watoto ambavyo vinamilikiwa na Serikali wanapata haki zote za msingi ikiwemo elimu ya msingi, sekondari, vyuo vikuu na elimu ya ufundi (VETA). Wanapomaliza wanapewa vifaa maalum vya kujiendeleza ili waweze kujiajiri wenyewe. Ahsante sana.

Name

Juliana Didas Masaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia watoto wa mitaani ambapo kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa?

Supplementary Question 2

MHE. JULIANA D. MASABURI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kumekuwa na wimbi kubwa la wazazi kuwafanyia vitendo vya kikatili watoto. Je, Serikali inampango gani wa kuwajengea watoto uwezo au uelewa mashuleni wa kujitetea pindi wanapopitia ukatili wa kijjinsia?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA,WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kukubaliana na hili, Serikali inatekeleza afua mbalimbali za kutoa elimu za malezi na makuzi, pamoja na elimu ambayo inakabiliana na ukatili dhidi ya watoto. Aidha, kuimarisha Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wanawake na watoto zilizopo ngazi zote nchini kwa ajili ya kuwa elimu wananchi wa jamii yetu.

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia watoto wa mitaani ambapo kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa?

Supplementary Question 3

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Watoto wa mitaani hususani watoto wa kiume wamekuwa wakipitia unyanyasaji na udhalilishaji wa kijinsia hususan suala la kulawitiwa. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuchukua hatua za haraka ikiwemo mabadiliko ya sheria ili kuweka sheria kali na za mfano kwa watu wanaotenda vitendo vya ulawiti kwa watoto?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA,WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kumekuwa na ukatili kwa watoto ambao wanalawitiwa. Serikali kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama, pamoja na maafisa wetu wa maendeleo na ustawi wa jamii, tunahakikisha kwamba, watuhumiwa wote ambao wanafanya vitendo vya ukatili kwa watoto wetu wanachukuliwa hatua kali pale inapostahiki. Ahsante.