Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 2 Community Development, Gender and Children Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum 34 2022-11-02

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia watoto wa mitaani ambapo kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA,WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: alijibu: -

Mheshimiwa Spika; kwa niaba ya Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum napenda kujibu swali la Mheshimiwa Taska Restituta Mbogo Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kumekuwepo na ongezeko la watoto wa mitaani hivi karibuni. Hii inatokana na sababu mbalimbali za kifamilia.

Mheshimiwa Spika, katika kupunguza watoto wa mitaani Serikali inafanya mikakati ifuatayo: -

Kuimarisha Kamati za Ulinzi na Usalama wa Wanawake na Watoto katika ngazi za jamii ambapo hadi sasa kuna jumla ya Kamati 18,186 katika ngazi za taifa, vile vile kutoa elimu kwa wazazi au walezi kuhusu malezi chanya ya watoto kupitia Ajenda ya Taifa ya uwajibikaji wa Wazazi katika malezi ya watoto kwenye familia. Aidha, Serikali kwa kushirikiana na wadau imekuwa ikifanya zoezi la kuwatambua na kuwaondoa watoto wanaoishi na kufanya kazi mtaani kwa kuwarudisha katika familia zao.

Mheshimiwa Spika, baadhi ya watoto ambao familia zao hazipatikani Serikali imekuwa ikiwapeleka katika makao ya watoto yanayomilikiwa na Serikali na yale yanayomilikiwa na taasisi binafsi, ambako wanapata huduma zote za msingi ikiwa ni pamoja na kuwaandalia mazingira ya kujitegemea kutokana na uwezeshaji wa elimu ya ufundi na mitaji ya kuanzia maisha.

Mheshimiwa Spika, natoa rai kwa viongozi na jamii kwa jumla kutimiza wajibu wao katika kuimarisha malezi chanya ya watoto katika familia.