Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: - Je, Serikali haioni haja ya kupunguza eneo la Hifadhi ya Msitu wa Mbiwe ili litumike kwa matumizi ya wananchi na shughuli za kiuchumi?

Supplementary Question 1

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana; nimeyapokea majibu ya Serikali. Kwa kuwa kwenye jibu la msingi amesema Serikali inaruhusu shughuli za kiuchumi kuweza kufanyika kwenye eneo la misitu zikifuata sheria, lakini sheria hizi zimekuwa ngumu sana kwa wachimbahi wadogo hawa kuweza kuzi-meet ili waweze kupata hivi vibali. Je, serikali haioni haja sasa kuweza kupunguza masharti ya kutoa vibali vya kuingia ndani ya misitu ili wananchi wetu hawa waweze kupata vibali hivyo waweze kufanya shughuli zao za uchumi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Serikali imekuwa inaendesha zoezi la kuweka beacon katika mipaka kati ya vijiji pamoja na hifadhi. Zoezi hili limeweza kufanyika katika Kata za Mafyeko, Kambikatoto pamoja na Matwiga. Zoezi hili limeweza kufanyika bila kuwashirikisha wananchi wa maeneo husika.

Je Serikali haioni haja sasa kuweza kuweka bikon zile upya katika maeneo yale ya mipaka ya asili ili wananchi hawa waweze kufanya shughuli zao vizuri bila kuleta taharuki?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Masache N. Kasaka, Mbunge wa Lupa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza aliloliongelea Mheshimiwa Mbunge, kuhusu kupunguza masharti ili kuruhusu wachimbaji wadogowadogo waweze kuingia katika maeneo yaliyohifadhiwa. Nimtaarifu tu Mbunge kwamba, masharti haya tuliyoyaweka, yanazingatia pia kuhifadhi maeneo ya misitu na masharti haya kwa wachimbaji wadogowadogo tumeyaweka ni machache sana.

Mheshimiwa spika, kwa mfano, kwa ridhaa yako napenda tu nielezee kuhusu suala la masharti ya wachimbaji wadogowadogo ambao wanapaswa kupata leseni. Pia wanatakiwa kufanya Environmental Protection Plan (EPP), ambayo huwa haifanani na EIA, ni masharti madogo ambayo yanamfanya mchimbaji aweze kufuzu ili aweze kupata kibali cha kuingia kuchimba. Kwa hiyo sisi tunaona masharti haya ni nafuu sana na tunaendelea kuhamasisha wananchi kwamba tunapohifadhi ni kwa ajili ya uhifadi endelevu na wakati huo huo tunaruhusu shughuli za uchimbaji ndani ya hifadhi.

Mheshimiwa Spika, kwenye hili zoezi la beacon, nimfahamishe tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tunapokuwa tunaweka mipaka, tunashirikisha pia Wizara ya Ardhi, ambapo wanakuwepo wapima ardhi ambao wanazisoma na kutafasiri ramani ambazo zinaonyesha ramani kamili ya hifadhi husika. Endapo kama kuna mgogoro uliojitokeza, basi nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge, kwamba tutawashirikisha tena Wizara ya Ardhi ili tujiridhishe na wananchi kwamba mipaka hii ni sahihi ama siyo sahihi. Kama itaonekana bikon zimewekwa nje ya mipaka hiyo, basi tutafanya marekebisho. Ahsante sana.