Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 2 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 33 2022-11-02

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: -

Je, Serikali haioni haja ya kupunguza eneo la Hifadhi ya Msitu wa Mbiwe ili litumike kwa matumizi ya wananchi na shughuli za kiuchumi?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii naomba kujibu swali la Mheshimiwa Masache N. Kasaka, Mbunge wa Lupa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, lengo la kuanzishwa hifadhi hiyo ni kulinda bayoanuai zilizomo ndani ya hifadhi ikiwemo vyanzo vya maji vinavyotumika kwa matumizi ya binadamu na wanyamapori.

Mheshimiwa Spika, Serikali haioni haja ya kupunguza eneo la hifadhi ya Msitu wa Mbiwe. Aidha, Sheria ya Misitu inaruhusu uchimbaji wa madini ndani ya hifadhi kwa kuzingatia kanuni na taratibu zilizopo kwa njia endelevu.