Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, nini mkakati wa Serikali kumaliza kero ya kukatikakatika kwa umeme Mikoa ya Kusini hasa Wilaya ya Masasi na Vijiji vyake?

Supplementary Question 1

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, lakini kumekuwa na uendelezaji mdogo sana wa miradi ya REA iliyopo kwenye Majimbo yote ya Mkoa wa Mtwara.

Swali la kwanza; pamoja na mikakati hii ya Serikali ya kutaka kuimarisha upatikanaji wa umeme kwenye wilaya zetu, ni lini sasa tutahakikisha Miradi ya REA iliyopo kwenye Majimbo yote ya Mkoa wa Mtwara inakamilika?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; tunataka kufahamu kwa uhakika kwa sababu mpaka sasa kuna vijiji zaidi ya 300 havijapatiwa umeme, wanaleta umeme wa grid kutoka Mtwara na hii wanayosema kutoka Mombika ili kuimarisha upatikanaji wa umeme kwenye Wilaya ya Masasi, nayo tunaomba kufahamu miradi hii itaanza kutekelezwa lini?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa David Cecil Mwambe kwa pamoja, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mikataba mingi ya REA III, round two ilikuwa inatakiwa kuisha Desemba, lakini kwa changamoto ambazo zilijitokeza ambazo tayari tulishazisema, muda wake wa kukamilika utaongezeka kidogo kulingana tofauti tofauti ya maeneo. Hata hivyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na Waheshimiwa Wabunge wengine wote kwamba Serikali kupitia Wizara ya Nishati inahakikisha kwamba mikataba hii inakamilika na wananchi wanapata umeme katika vijiji vyao, kwa sababu pesa ipo na usimamizi unaendelea kufanyika wa karibu. Kwa hiyo, tutaendelea kulisimamia hili ili umeme uweze kupatikana katika maeneo yetu.

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, nini mkakati wa Serikali kumaliza kero ya kukatikakatika kwa umeme Mikoa ya Kusini hasa Wilaya ya Masasi na Vijiji vyake?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY M. JUMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ni miezi mitatu sasa katika Wilaya ya Kyela, umeme haupatikani mchana. Je, ni lini wananchi wa Kyela watajisikia kwamba nao wana haki ya kupata umeme asubuhi na mchana?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Jumbe, Mbunge wa Kyela kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba baada ya hapa nikafuatilie ili kufahamu kwa nini Mheshimiwa Mbunge katika jimbo lake kwa miezi mitatu hakupatikani umeme mchana. Ninachofahamu ni kwamba kwa sababu ya upungufu wa umeme kumekuwa na kupungua kwa umeme kwenye baadhi ya maeneo, lakini jambo la kwamba miezi mitatu mchana wote hakuna, hilo ni jambo la kufuatilia, halafu tutashirikiana na Mheshimiwa Mbunge ili tuweze kutatua changamoto hiyo.

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, nini mkakati wa Serikali kumaliza kero ya kukatikakatika kwa umeme Mikoa ya Kusini hasa Wilaya ya Masasi na Vijiji vyake?

Supplementary Question 3

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Naomba Serikali ituambie hususani Wizara ya Nishati, kuna kigugumizi gani hasa katika suala la REA? Maana yake kumekuwa na changamoto kubwa sana kwa hawa Wakandarasi hawatoi ushirikiano, lakini hawashughuliki kabisa na miradi ile inayotakiwa ifanyike kule. Mfano kwenye jimbo langu ule mkataba uliopita haujatekelezwa hata katika kijiji kimoja. Sasa Serikali ina kigugumizi gani katika jambo hili, ituambie ukweli?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mchungahela, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, niombe kupata ushirikiano wa Waheshimiwa Wabunge kwa sababu ni case by case kwamba Mkandarasi hana ushirikiano mzuri na Mbunge. Wako Waheshimiwa Wabunge wengine ambao wanatoa sifa nzuri na recommendation nzuri kwa wakandarasi waliokuwa nao kwamba wanatoa ushirikiano. Kwa hiyo, naomba kwa wale ambao wanapata changamoto ya ushirikiano, basi tuwasiliane ili tuweze kutatua changamoto hizo katika maeneo yao ili tuweze kuhakikisha kwamba miradi hii inakamilika kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, kwenye eneo lingine, tuwasiliane pia na kupeana taarifa na updates sahihi za ni lini umeme umewaka wapi na utawashwa wapi na pale ambapo tunaona kuna changamoto za ucheleweshaji usiokuwa na sababu kwa pamoja tuweze kushirikiana na kuchukua hatua ili tufikie azma ya kuwasha umeme katika vijiji vyetu vyote kwa kadri ya mikataba, lakini na lengo la Serikali Awamu ya Sita inaongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan.

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, nini mkakati wa Serikali kumaliza kero ya kukatikakatika kwa umeme Mikoa ya Kusini hasa Wilaya ya Masasi na Vijiji vyake?

Supplementary Question 4

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Naomba kuuliza kuhusu suala la Mkandarasi wa REA katika Mkoa wetu wa Songwe. Nafikiri hili tatizo Waziri analifahamu na binafsi nimekwenda ofisini kwake mara kadhaa kuhusu huyo Mkandarasi. Kwa kifupi huyu mkandarasi ana kiburi, mpaka sasa hivi amewasha vijiji vitano tu mkoa mzima na ana majibu ya jeuri, Waziri mwenyewe ameshuhudia. Sasa nini mkakati wa Wizara au Waziri yuko tayari kwenda Songwe kuonana na huyu mkandarasi kuhusu tatizo la REA, Mkoa wa Songwe? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwenisongole, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mkandarasi anayetekeleza mradi wa REA III, Round Two katika Mkoa wa Songwe, ni mkandarasi anayeitwa Derm Electric ambaye pia anafanya kazi hiyo katika Mkoa wa Dodoma. Mkandarasi huyu siyo hohehahe, siyo legelege, ni mojawapo ya wakandarasi ambao tunawatarajia wafanye kazi nzuri. Changamoto ambayo Mheshimiwa Mbunge ameisema tumeshaanza kuifanyia kazi na tutaendelea kusukumana na kusimamiana ili kazi hizo zote za maeneo husika ziweke kukamilika kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, tayari tumeshapanga kikao na wakandarasi hawa, mwishoni mwa mwezi huu ili tuweze kwa pamoja changamoto ambazo zinatokea kwa upande wao ili tuweze kuzitatua na kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: - Je, nini mkakati wa Serikali kumaliza kero ya kukatikakatika kwa umeme Mikoa ya Kusini hasa Wilaya ya Masasi na Vijiji vyake?

Supplementary Question 5

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, naungana na Wabunge wenzangu, mkandarasi ambaye amepewa Miradi ya REA katika Wilaya za Mvomero, Ulanga, Malinyi, Kilosa mpaka sasa hajawasha umeme katika kijiji hata kimoja. Sasa na hilo nalo wananchi wa Jimbo la Mikumi wanataka kujua nini kauli ya Serikali kwenye hili?

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba baada ya hapa niwasiliane naye ili nijue changamoto hasa kwenye eneo lake ni sehemu gani anasema hakujawasha hata kijiji kimoja. Baada ya hapo tutafuatilia kujua changamoto iko wapi, pengine ni kwa sababu mkandarasi anakuwa na maeneo manne, matano, sita pengine kaanzia kwingine kwake hajafika. Zile hatua za awali za kuhakiki mipaka, kuhakiki maeneo ya kuweka miundombinu na kuhakiki urefu, tayari zimeshafanyika kwenye maeneo yote inafuata kuweka nguzo, kuvuta wires na sasa kuwasha umeme. Kwa hiyo, tukishafuatilia tutajua hatua gani imefikiwa katika eneo lake, lakini kazi hiyo lazima ifanyike na kukamilika.