Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 25 2022-11-02

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. CECIL D. MWAMBE aliuliza: -

Je, nini mkakati wa Serikali kumaliza kero ya kukatikakatika kwa umeme Mikoa ya Kusini hasa Wilaya ya Masasi na Vijiji vyake?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Cecil David Mwambe, Mbunge wa Ndanda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hali ya upatikanaji wa umeme katika Mkoa wa Mtwara imeendelea kuimarika na kuwa ya kuridhisha ukilinganishwa na kipindi cha nyuma. Serikali inao mkakati wa dhati wa kumaliza changamoto hii kwa mikoa ya Kusini na maeneo mengine ya Tanzania nzima.

Mheshimiwa Spika, ili kuondoa changamoto hii, Serikali imetenga jumla ya shilingi milioni 600 kwa ajili ya kurekebisha miundombinu katika line za Newala, Nyangao, Masasi na Mahuta. Aidha, jumla ya shilingi bilioni 2.2 zimetengwa kwa ajili ya kujenga njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 kutoka Nanganga hadi Masasi. Pia, jumla ya shilingi bilioni mbili zimetengwa kuweka transfoma kubwa kati ya Tunduru na Namtumbo ili kupata umeme mkubwa kutoka Ruvuma bila kuathiri watumiaji wengine.

Mheshimiwa Spika, katika mpango wa kudumu wa kuimarisha Gridi ya Taifa, Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 250 kujenga Gridi ya Taifa kutoka Songea – Tunduru – hadi Masasi. Kwa mwaka 2022/2023 Serikali imetenga jumla ya shilingi bilioni 66.7 kuanza ujenzi wa njia hiyo.