Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: - Je, nini kauli ya Serikali juu ya mapunjo ya fidia kwa wananchi walioathirika na mlipuko wa mabomu Mbagala?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Spika, kutokana na majibu hayo ya Serikali: Je, Serikali haioni ipo haja sasa ya kutoa ufafanuzi kwa wananchi hao ya tofauti kati ya fidia na kifuta machozi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili: Je, kutokana na malalamiko ya wananchi hao kuwa mengi, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuongozana nami jimboni ili kwenda kuwasikiliza wananchi hao na hatimaye kutatua matatizo hayo? (Makofi)

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE NA URATIBU): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Chaurembo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nianze na swali la pili kwamba niko tayari wakati wowote kufuatana na Mheshimiwa Mbunge ili kwenda kuwasikiliza wananchi. Bahati nzuri nilipata fursa ya kukutana na baadhi yao na kwa niaba yangu alikutana nao Mheshimiwa Jafo Dar es Salaam, na tulipokea barua yao na baadhi yao tunaendelea kuwasiliana nao. Tutafanya hivyo ili tukawasilikilize kule kule kwa sababu ndiyo kazi ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ni ufafanuzi wa tofauti ya maafa au fidia na kifuta machozi. Maafa yanasababisha na majanga, majanga na huwa si jambo lililopangwa au kutarajiwa, majanga yanaweza kutokana na nguvu za asili, inaweza ikawa na mafuriko, au Tsunami, pia majanga yanaweza yakatokana na matokeo mbalimbali ya nguvu ambazo siyo za kawaida. Inaweza ikawa ni mlipuko wa magonjwa, na yenyewe hayo pia ni majanga.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, yanapotokea maafa, huwezi ukayawekea utaratibu wa kulipa fidia. Kwa hiyo, hakuna utaratibu wa fidia kwa majanga, bali ambacho hutokea, jamii au Serikali huweza kutoa kifuta machozi au mkono wa pole kwa walioathirika. Kwa hiyo, Serikali ilifanya hivyo na iliwalipa kifuta machozi. Pia Serikali ililipa kifuta machozi kiasi cha Shilingi 17,464,944,954/=, fedha hizi ni nyingi.

Mheshimiwa Spika, pia Serikali ilishughulikia mazishi ya wale ambao walifariki katika tukio lile. Naomba kuwasilisha.