Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 9 Sitting 2 Policy, Coordination and Parliamentary Affairs Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge 21 2022-11-02

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: -

Je, nini kauli ya Serikali juu ya mapunjo ya fidia kwa wananchi walioathirika na mlipuko wa mabomu Mbagala?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE NA URATIBU) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Jafari Chaurembo, Mbunge wa Mbagala, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali ilitoa mkono wa pole na siyo fidia, kwa wananchi 12,647 waliothirika na milipuko ya mabomu iliyotokea tarehe 29 Aprili, 2009 katika Kambi ya JWTZ Mbagala. Malipo hayo, yalitolewa kwa awamu sita kuanzia mwaka 2009 hadi 2020. Vile vile, Serikali ilitoa kifuta machozi pamoja na kugharamia huduma za mazishi kwa familia 29 zilizopoteza wapendwa wao kutokana na milipuko hiyo ya mabomu ya Mbagala.

Mheshimiwa Spika, zoezi la kutoa mkono wa pole kwa waathirika lilisitishwa rasmi na Serikali mnamo mwezi Machi, 2020 baada ya walengwa wote waliokusudiwa kujitokeza na kulipwa.