Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA K.n.y. MHE. ASSA N. MAKANIKA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Mwandiga – Chankele – Mwamgongo hadi Kagunga?

Supplementary Question 1

MHE. ZAINAB A. KATIMBA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa majibu ya Serikali yanayotia faraja. Nina swali moja la nyongeza. Naomba kufahamu na kauli ya Serikali kuhusiana na kukamilika kwa ujenzi wa barabara hii ifikapo mwaka 2025.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zainab Katimba, Mbunge wa Viti Maalum, Kigoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii ipo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi tunayoitekeleza sasa hivi na imeeleza wazi kwamba lazima tuifanyie usanifu wa kina. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Mheshimiwa Makanika ambaye amekuwa akiifuatilia sana hii barabara kwamba tutahakikisha tunaifungua yote na baada ya hapo tutaanza kuifanyia usanifu wa kina baada ya kukamilisha upembuzi yakinifu wa barabara hii.

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA K.n.y. MHE. ASSA N. MAKANIKA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Mwandiga – Chankele – Mwamgongo hadi Kagunga?

Supplementary Question 2

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kuniona. Kipande cha barabara kinachotoka Uvinza kuelekea Malagarasi ujenzi wake unasuasua sana kwa muda mrefu. Napenda kujua nini tatizo la Serikali kufanya kipande hicho cha barabara kisikamilike?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kilumbe Ng’enda, Mbunge wa Kigoma Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii ilikuwa inasuasua, lakini sasa nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii ya Uvinza hadi Malagarasi yenye urefu wa kilometa 51, kasi imeongezeka baada ya kuondoa changamoto zilizokuwepo. Ni matumaini yetu kwamba Mkandarasi huyu ataikamilisha barabara hii ndani ya wakati. Ahsante.

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA K.n.y. MHE. ASSA N. MAKANIKA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Mwandiga – Chankele – Mwamgongo hadi Kagunga?

Supplementary Question 3

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Naomba kumwuliza Mheshimiwa Waziri, ni lini Serikali itafanya upanuzi wa barabara ya Moshi – Arusha kuanzia Tengeru – USA – Moshi Mjini – Himo mpaka Holili?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE):
Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Priscus Tarimo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii imetengewa fedha kuijenga, kwa maana ya kuikarabati, ikiwa ni pamoja ya kujenga daraja la Mto Karanga. Kwa hiyo, taratibu zinaendelea ili kuanza kuijenga hii barabara ikiwa ni kuikarabati sasa kwa kiwango kikubwa kwa mwaka huu wa fedha. Ahsante.